< Zaburi 68 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Mungu na ainuke, watesi wake watawanyike, adui zake na wakimbie mbele zake.
“For the leader of the music. A psalm of David.” Let God arise, and his enemies are scattered, And they who hate him flee before him!
2 Kama vile moshi upeperushwavyo na upepo, vivyo hivyo uwapeperushe mbali, kama vile nta iyeyukavyo kwenye moto, vivyo hivyo waovu na waangamie mbele za Mungu.
As smoke is dispersed, so thou dispersest them; As wax melteth before the fire, So perish the wicked before the face of God.
3 Bali wenye haki na wafurahi, washangilie mbele za Mungu, wafurahi na kushangilia.
But the righteous are glad and rejoice in his presence, Yea, they exult exceedingly.
4 Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake, mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu: jina lake ni Bwana, furahini mbele zake.
Sing unto God; sing praises to his name! Prepare a way for him who rideth through the desert! Jehovah is his name; be joyful in his presence!
5 Baba wa yatima, mtetezi wa wajane, ni Mungu katika makao yake matakatifu.
The father of the fatherless, and the protector of the widow, Is God in his holy habitation.
6 Mungu huwaweka wapweke katika jamaa, huwaongoza wafungwa wakiimba, bali waasi huishi katika nchi kame.
God causeth the forsaken to dwell in houses; He leadeth forth to prosperity them that are bound; But the rebellious shall dwell in a barren land.
7 Ee Mungu, ulipowatangulia watu wako, ulipopita nyikani,
O God! when thou didst go before thy people, When thou didst march through the wilderness. (Pause)
8 dunia ilitikisika, mbingu zikanyesha mvua, mbele za Mungu, Yule wa Sinai, mbele za Mungu, Mungu wa Israeli.
The earth quaked, and the heavens dropped at the presence of God; This Sinai trembled at the presence of God, the God of Israel.
9 Ee Mungu, ulinyesha mvua nyingi na kuiburudisha ardhi iliyokuwa imechoka.
Thou, O God! didst send a plentiful rain; Thou didst strengthen thy wearied inheritance.
10 Ee Mungu, watu wako waliishi huko, nawe kwa wingi wa utajiri wako uliwapa maskini mahitaji yao.
Thy people established themselves in the land; Thou, O God! in thy goodness, didst prepare it for the needy!
11 Bwana alitangaza neno, waliolitangaza neno hilo walikuwa kundi kubwa:
The Lord gave the song of victory Of the maidens publishing glad tidings to the mighty host.
12 “Wafalme na majeshi walikimbia upesi, watu waliobaki kambini waligawana nyara.
“The kings with their armies have fled, —have fled! And the matron at home divideth the spoil.
13 Hata ulalapo katikati ya mioto ya kambini, mabawa ya njiwa wangu yamefunikwa kwa fedha, manyoya yake kwa dhahabu ingʼaayo.”
Truly ye may repose yourselves in the stalls, Like the wings of a dove covered with silver, And her feathers with shining gold.”
14 Wakati Mwenyezi alipowatawanya wafalme katika nchi, ilikuwa kama theluji iliyoanguka juu ya Salmoni.
When the Most High destroyed the kings in the land, It was white [[with their bones]] like Salmon.
15 Milima ya Bashani ni milima iliyotukuka, milima ya Bashani ina vilele vilivyochongoka.
Ye lofty hills, ye hills of Bashan, Ye many-topped hills, ye hills of Bashan,
16 Enyi milima yenye vilele vilivyochongoka, kwa nini mnakazia macho kwa wivu, katika mlima Mungu anaochagua kutawala, ambako Bwana mwenyewe ataishi milele?
Why frown ye, ye many-topped hills, At the hill in which God is pleased to dwell, In which Jehovah will dwell for ever?
17 Magari ya Mungu ni makumi ya maelfu, na maelfu ya maelfu; Bwana amekuja kutoka Sinai hadi katika patakatifu pake.
The chariots of God are myriads, yea, thousands of thousands; The Lord is in the midst of them, as upon Sinai, in the sanctuary.
18 Ulipopanda juu, uliteka mateka, ukapokea vipawa kutoka kwa wanadamu, hata kutoka kwa wale walioasi, ili wewe, Ee Bwana Mungu, upate kuishi huko.
Thou hast ascended on high, Thou hast led captive the vanquished, Thou hast received gifts among men, Even the rebellious, that here thou mightst dwell, O LORD God!
19 Sifa apewe Bwana, Mungu Mwokozi wetu, ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu.
Praised be the Lord daily! When we are heavy-laden, the Mighty One is our help.
20 Mungu wetu ni Mungu aokoaye, Bwana Mwenyezi hutuokoa na kifo.
Our God is a God of salvation; From the Lord Jehovah cometh deliverance from death.
21 Hakika Mungu ataponda vichwa vya adui zake, vichwa vya hao waendao katika njia za dhambi.
But God smiteth the head of his enemies, Even the hairy crowns of those who go on in their iniquity.
22 Bwana alisema, “Nitawarudisha kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari,
“I will bring them back,” saith the Lord, “from Bashan; I will bring them back from the deep sea;
23 ili uweze kuchovya miguu yako katika damu ya adui zako, huku ndimi za mbwa wako zikiwa na fungu lake.”
That thy foot may be dipped in their blood, That thy dogs may drink the blood of thine enemies.”
24 Ee Mungu, maandamano yako yameonekana, maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, yakielekea patakatifu pake.
We have seen thy procession, O God! The procession of my God, my king, to his sanctuary!
25 Mbele wako waimbaji, baada yao wapiga vinanda, pamoja nao wako wanawali wakipiga matari.
The singers go before, the minstrels follow, Amidst damsels playing on timbrels.
26 Msifuni Mungu katika kusanyiko kubwa, msifuni Bwana katika kusanyiko la Israeli.
Praise ye God in your assemblies; Praise the Lord, all ye from the fountain of Israel!
27 Liko kabila dogo la Benyamini likiwaongoza, wakifuatwa na kundi kubwa la watawala wa Yuda, hatimaye watawala wa Zabuloni na Naftali.
Here is Benjamin, the youngest, and his leaders; The chiefs of Judah, and their band; The chiefs of Zebulon, and the chiefs of Naphtali.
28 Ee Mungu, amuru uwezo wako, Ee Mungu tuonyeshe nguvu zako, kama ulivyofanya hapo awali.
Thy God has ordained thy strength, [[O Israel!]] Show forth thy might, O God! thou who hast wrought for us!
29 Kwa sababu ya Hekalu lako Yerusalemu wafalme watakuletea zawadi.
Because of thy temple in Jerusalem Shall kings bring presents to thee.
30 Mkemee mnyama aliyeko kwenye manyasi, kundi la mafahali katikati ya ndama za mataifa. Na walete minara ya madini ya fedha wakinyenyekea. Tawanya mataifa yapendayo vita.
Rebuke the wild beast of the reeds, The multitude of bulls with the calves of the nations, So that they shall cast themselves down with masses of silver; Scatter thou the nations that delight in war!
31 Wajumbe watakuja kutoka Misri, Kushi atajisalimisha kwa Mungu.
Princes shall come out of Egypt; Ethiopia shall haste with outstretched hands to God.
32 Mwimbieni Mungu, enyi falme za dunia, mwimbieni Bwana sifa,
Ye kingdoms of the earth, sing unto God; Sing praises to Jehovah;
33 mwimbieni sifa yeye apandaye mbingu za kale zilizo juu, yeye angurumaye kwa sauti kuu.
To him who rideth upon the ancient heaven of heavens! Behold, he uttereth his voice, his mighty voice!
34 Tangazeni uwezo wa Mungu, ambaye fahari yake iko juu ya Israeli, ambaye uwezo wake uko katika anga.
Give glory to God, Whose majesty is in Israel, and whose might is in the clouds!
35 Ee Mungu, wewe unatisha katika mahali patakatifu pako, Mungu wa Israeli huwapa watu wake uwezo na nguvu. Mungu Asifiwe!
Terrible art thou, O God! from thy sanctuary! The God of Israel giveth strength and power to his people. Praised be God!

< Zaburi 68 >