< Zaburi 68 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Mungu na ainuke, watesi wake watawanyike, adui zake na wakimbie mbele zake.
For the Leader. A Psalm of David, a Song. Let God arise, let His enemies be scattered; and let them that hate Him flee before Him.
2 Kama vile moshi upeperushwavyo na upepo, vivyo hivyo uwapeperushe mbali, kama vile nta iyeyukavyo kwenye moto, vivyo hivyo waovu na waangamie mbele za Mungu.
As smoke is driven away, so drive them away; as wax melteth before the fire, so let the wicked perish at the presence of God.
3 Bali wenye haki na wafurahi, washangilie mbele za Mungu, wafurahi na kushangilia.
But let the righteous be glad, let them exult before God; yea, let them rejoice with gladness.
4 Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake, mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu: jina lake ni Bwana, furahini mbele zake.
Sing unto God, sing praises to His name; extol Him that rideth upon the skies, whose name is the LORD; and exult ye before Him.
5 Baba wa yatima, mtetezi wa wajane, ni Mungu katika makao yake matakatifu.
A father of the fatherless, and a judge of the widows, is God in His holy habitation.
6 Mungu huwaweka wapweke katika jamaa, huwaongoza wafungwa wakiimba, bali waasi huishi katika nchi kame.
God maketh the solitary to dwell in a house; He bringeth out the prisoners into prosperity; the rebellious dwell but in a parched land.
7 Ee Mungu, ulipowatangulia watu wako, ulipopita nyikani,
O God, when Thou wentest forth before Thy people, when Thou didst march through the wilderness; (Selah)
8 dunia ilitikisika, mbingu zikanyesha mvua, mbele za Mungu, Yule wa Sinai, mbele za Mungu, Mungu wa Israeli.
The earth trembled, the heavens also dropped at the presence of God; even yon Sinai trembled at the presence of God, the God of Israel.
9 Ee Mungu, ulinyesha mvua nyingi na kuiburudisha ardhi iliyokuwa imechoka.
A bounteous rain didst Thou pour down, O God; when Thine inheritance was weary, Thou didst confirm it.
10 Ee Mungu, watu wako waliishi huko, nawe kwa wingi wa utajiri wako uliwapa maskini mahitaji yao.
Thy flock settled therein; Thou didst prepare in Thy goodness for the poor, O God.
11 Bwana alitangaza neno, waliolitangaza neno hilo walikuwa kundi kubwa:
The Lord giveth the word; the women that proclaim the tidings are a great host.
12 “Wafalme na majeshi walikimbia upesi, watu waliobaki kambini waligawana nyara.
Kings of armies flee, they flee; and she that tarrieth at home divideth the spoil.
13 Hata ulalapo katikati ya mioto ya kambini, mabawa ya njiwa wangu yamefunikwa kwa fedha, manyoya yake kwa dhahabu ingʼaayo.”
When ye lie among the sheepfolds, the wings of the dove are covered with silver, and her pinions with the shimmer of gold.
14 Wakati Mwenyezi alipowatawanya wafalme katika nchi, ilikuwa kama theluji iliyoanguka juu ya Salmoni.
When the Almighty scattereth kings therein, it snoweth in Zalmon.
15 Milima ya Bashani ni milima iliyotukuka, milima ya Bashani ina vilele vilivyochongoka.
A mountain of God is the mountain of Bashan; a mountain of peaks is the mountain of Bashan.
16 Enyi milima yenye vilele vilivyochongoka, kwa nini mnakazia macho kwa wivu, katika mlima Mungu anaochagua kutawala, ambako Bwana mwenyewe ataishi milele?
Why look ye askance, ye mountains of peaks, at the mountain which God hath desired for His abode? Yea, the LORD will dwell therein for ever.
17 Magari ya Mungu ni makumi ya maelfu, na maelfu ya maelfu; Bwana amekuja kutoka Sinai hadi katika patakatifu pake.
The chariots of God are myriads, even thousands upon thousands; the Lord is among them, as in Sinai, in holiness.
18 Ulipopanda juu, uliteka mateka, ukapokea vipawa kutoka kwa wanadamu, hata kutoka kwa wale walioasi, ili wewe, Ee Bwana Mungu, upate kuishi huko.
Thou hast ascended on high, Thou hast led captivity captive; Thou hast received gifts among men, yea, among the rebellious also, that the LORD God might dwell there.
19 Sifa apewe Bwana, Mungu Mwokozi wetu, ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu.
Blessed be the Lord, day by day He beareth our burden, even the God who is our salvation. (Selah)
20 Mungu wetu ni Mungu aokoaye, Bwana Mwenyezi hutuokoa na kifo.
God is unto us a God of deliverances; and unto GOD the Lord belong the issues of death.
21 Hakika Mungu ataponda vichwa vya adui zake, vichwa vya hao waendao katika njia za dhambi.
Surely God will smite through the head of His enemies, the hairy scalp of him that goeth about in his guiltiness.
22 Bwana alisema, “Nitawarudisha kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari,
The Lord said: 'I will bring back from Bashan, I will bring them back from the depths of the sea;
23 ili uweze kuchovya miguu yako katika damu ya adui zako, huku ndimi za mbwa wako zikiwa na fungu lake.”
That thy foot may wade through blood, that the tongue of thy dogs may have its portion from thine enemies.'
24 Ee Mungu, maandamano yako yameonekana, maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, yakielekea patakatifu pake.
They see Thy goings, O God, even the goings of my God, my King, in holiness.
25 Mbele wako waimbaji, baada yao wapiga vinanda, pamoja nao wako wanawali wakipiga matari.
The singers go before, the minstrels follow after, in the midst of damsels playing upon timbrels.
26 Msifuni Mungu katika kusanyiko kubwa, msifuni Bwana katika kusanyiko la Israeli.
'Bless ye God in full assemblies, even the Lord, ye that are from the fountain of Israel.'
27 Liko kabila dogo la Benyamini likiwaongoza, wakifuatwa na kundi kubwa la watawala wa Yuda, hatimaye watawala wa Zabuloni na Naftali.
There is Benjamin, the youngest, ruling them, the princes of Judah their council, the princes of Zebulun, the princes of Naphtali.
28 Ee Mungu, amuru uwezo wako, Ee Mungu tuonyeshe nguvu zako, kama ulivyofanya hapo awali.
Thy God hath commanded thy strength; be strong, O God, Thou that hast wrought for us
29 Kwa sababu ya Hekalu lako Yerusalemu wafalme watakuletea zawadi.
Out of Thy temple at Jerusalem, whither kings shall bring presents unto Thee.
30 Mkemee mnyama aliyeko kwenye manyasi, kundi la mafahali katikati ya ndama za mataifa. Na walete minara ya madini ya fedha wakinyenyekea. Tawanya mataifa yapendayo vita.
Rebuke the wild beast of the reeds, the multitude of the bulls, with the calves of the peoples, every one submitting himself with pieces of silver; He hath scattered the peoples that delight in war!
31 Wajumbe watakuja kutoka Misri, Kushi atajisalimisha kwa Mungu.
Nobles shall come out of Egypt; Ethiopia shall hasten to stretch out her hands unto God.
32 Mwimbieni Mungu, enyi falme za dunia, mwimbieni Bwana sifa,
Sing unto God, ye kingdoms of the earth; O sing praises unto the Lord; (Selah)
33 mwimbieni sifa yeye apandaye mbingu za kale zilizo juu, yeye angurumaye kwa sauti kuu.
To Him that rideth upon the heavens of heavens, which are of old; lo, He uttereth His voice, a mighty voice.
34 Tangazeni uwezo wa Mungu, ambaye fahari yake iko juu ya Israeli, ambaye uwezo wake uko katika anga.
Ascribe ye strength unto God; His majesty is over Israel, and His strength is in the skies.
35 Ee Mungu, wewe unatisha katika mahali patakatifu pako, Mungu wa Israeli huwapa watu wake uwezo na nguvu. Mungu Asifiwe!
Awful is God out of thy holy places; the God of Israel, He giveth strength and power unto the people; blessed be God.

< Zaburi 68 >