< Zaburi 68 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Mungu na ainuke, watesi wake watawanyike, adui zake na wakimbie mbele zake.
Til Sangmesteren. Af David. En Salme. En Sang.
2 Kama vile moshi upeperushwavyo na upepo, vivyo hivyo uwapeperushe mbali, kama vile nta iyeyukavyo kwenye moto, vivyo hivyo waovu na waangamie mbele za Mungu.
Naar Gud staar op, da splittes hans Fjender, hans Avindsmænd flyr for hans Aasyn,
3 Bali wenye haki na wafurahi, washangilie mbele za Mungu, wafurahi na kushangilia.
som Røg henvejres, saa henvejres de; som Voks, der smelter for Ild, gaar gudløse til Grunde for Guds Aasyn.
4 Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake, mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu: jina lake ni Bwana, furahini mbele zake.
Men retfærdige frydes og jubler med Glæde og Fryd for Guds Aasyn.
5 Baba wa yatima, mtetezi wa wajane, ni Mungu katika makao yake matakatifu.
Syng for Gud, lovsyng hans Navn, hyld ham, der farer frem gennem Ørknerne! HERREN er hans Navn, jubler for hans Aasyn,
6 Mungu huwaweka wapweke katika jamaa, huwaongoza wafungwa wakiimba, bali waasi huishi katika nchi kame.
faderløses Fader, Enkers Værge, Gud i hans hellige Bolig,
7 Ee Mungu, ulipowatangulia watu wako, ulipopita nyikani,
Gud, som bringer ensomme hjem, fører Fanger ud til Lykke; men genstridige bor i tørre Egne.
8 dunia ilitikisika, mbingu zikanyesha mvua, mbele za Mungu, Yule wa Sinai, mbele za Mungu, Mungu wa Israeli.
Da du drog ud, o Gud, i Spidsen for dit Folk, skred frem gennem Ørkenen, (Sela) da rystede Jorden,
9 Ee Mungu, ulinyesha mvua nyingi na kuiburudisha ardhi iliyokuwa imechoka.
ja, Himlen dryppede for Guds Aasyn, for Guds Aasyn, Israels Guds.
10 Ee Mungu, watu wako waliishi huko, nawe kwa wingi wa utajiri wako uliwapa maskini mahitaji yao.
Regn i Strømme lod du falde, o Gud, din vansmægtende Arvelod styrkede du;
11 Bwana alitangaza neno, waliolitangaza neno hilo walikuwa kundi kubwa:
din Skare tog Bolig der, for de arme sørged du, Gud, i din Godhed.
12 “Wafalme na majeshi walikimbia upesi, watu waliobaki kambini waligawana nyara.
Ord lægger Herren de Kvinder i Munden, som bringer Glædesbud, en talrig Hær:
13 Hata ulalapo katikati ya mioto ya kambini, mabawa ya njiwa wangu yamefunikwa kwa fedha, manyoya yake kwa dhahabu ingʼaayo.”
»Hærenes Konger flyr, de flyr, Husets Frue uddeler Bytte.
14 Wakati Mwenyezi alipowatawanya wafalme katika nchi, ilikuwa kama theluji iliyoanguka juu ya Salmoni.
Vil I da blive imellem Foldene? Duens Vinger dækkes af Sølv, dens Fjedre af gulgrønt Guld.
15 Milima ya Bashani ni milima iliyotukuka, milima ya Bashani ina vilele vilivyochongoka.
Da den Almægtige splittede Kongerne der, faldt der Sne paa Zalmon.«
16 Enyi milima yenye vilele vilivyochongoka, kwa nini mnakazia macho kwa wivu, katika mlima Mungu anaochagua kutawala, ambako Bwana mwenyewe ataishi milele?
Et Gudsbjerg er Basans Bjerg, et Bjerg med spidse Tinder er Basans Bjerg;
17 Magari ya Mungu ni makumi ya maelfu, na maelfu ya maelfu; Bwana amekuja kutoka Sinai hadi katika patakatifu pake.
Hvi skæver I Bjerge med spidse Tinder til Bjerget, Gud ønsked til Bolig, hvor HERREN ogsaa vil bo for evigt?
18 Ulipopanda juu, uliteka mateka, ukapokea vipawa kutoka kwa wanadamu, hata kutoka kwa wale walioasi, ili wewe, Ee Bwana Mungu, upate kuishi huko.
Titusinder er Guds Vogne, tusinde Gange tusinde, HERREN kom fra Sinaj til Helligdommen.
19 Sifa apewe Bwana, Mungu Mwokozi wetu, ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu.
Du steg op til det høje, du bortførte Fanger, Gaver tog du blandt Mennesker, ogsaa iblandt de genstridige, at du maatte bo der, HERRE, o Gud.
20 Mungu wetu ni Mungu aokoaye, Bwana Mwenyezi hutuokoa na kifo.
Lovet være Herren! Fra Dag til Dag bærer han vore Byrder; Gud er vor Frelse. (Sela)
21 Hakika Mungu ataponda vichwa vya adui zake, vichwa vya hao waendao katika njia za dhambi.
En Gud til Frelse er Gud for os, hos den Herre HERREN er Udgange fra Døden.
22 Bwana alisema, “Nitawarudisha kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari,
Men Fjendernes Hoveder knuser Gud, den gudløses Isse, der vandrer i sine Synder.
23 ili uweze kuchovya miguu yako katika damu ya adui zako, huku ndimi za mbwa wako zikiwa na fungu lake.”
Herren har sagt: »Jeg henter dem hjem fra Basan, henter dem hjem fra Havets Dyb,
24 Ee Mungu, maandamano yako yameonekana, maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, yakielekea patakatifu pake.
at din Fod maa vade i Blod, dine Hundes Tunger faa del i Fjenderne.«
25 Mbele wako waimbaji, baada yao wapiga vinanda, pamoja nao wako wanawali wakipiga matari.
Se paa Guds Højtidstog, min Guds, min Konges Højtidstog ind i Helligdommen!
26 Msifuni Mungu katika kusanyiko kubwa, msifuni Bwana katika kusanyiko la Israeli.
Sangerne forrest, saa de, der spiller, i Midten unge Piger med Pauker:
27 Liko kabila dogo la Benyamini likiwaongoza, wakifuatwa na kundi kubwa la watawala wa Yuda, hatimaye watawala wa Zabuloni na Naftali.
»Lover Gud i Festforsamlinger, Herren, I af Israels Kilde!«
28 Ee Mungu, amuru uwezo wako, Ee Mungu tuonyeshe nguvu zako, kama ulivyofanya hapo awali.
Der er liden Benjamin forrest, Judas Fyrster i Flok, Zebulons Fyrster, Naftalis Fyrster.
29 Kwa sababu ya Hekalu lako Yerusalemu wafalme watakuletea zawadi.
Opbyd, o Gud, din Styrke, styrk, hvad du gjorde for os, o Gud!
30 Mkemee mnyama aliyeko kwenye manyasi, kundi la mafahali katikati ya ndama za mataifa. Na walete minara ya madini ya fedha wakinyenyekea. Tawanya mataifa yapendayo vita.
For dit Tempels Skyld skal Konger bringe dig Gaver i Jerusalem.
31 Wajumbe watakuja kutoka Misri, Kushi atajisalimisha kwa Mungu.
Tru ad Dyret i Sivet, Tyreflokken, Folkeslags Herrer, saa de hylder dig med deres Sølvstykker. Adsplit Folkeslag, der elsker Strid!
32 Mwimbieni Mungu, enyi falme za dunia, mwimbieni Bwana sifa,
De kommer med Olie fra Ægypten, Ætioperne iler til Gud med fulde Hænder.
33 mwimbieni sifa yeye apandaye mbingu za kale zilizo juu, yeye angurumaye kwa sauti kuu.
I Jordens Riger, syng for Gud, lovsyng HERREN;
34 Tangazeni uwezo wa Mungu, ambaye fahari yake iko juu ya Israeli, ambaye uwezo wake uko katika anga.
hyld ham, der farer frem paa Himlenes Himle, de gamle! Se, han løfter sin Røst, en vældig Røst.
35 Ee Mungu, wewe unatisha katika mahali patakatifu pako, Mungu wa Israeli huwapa watu wake uwezo na nguvu. Mungu Asifiwe!
Giv Gud Ære! Over Israel er hans Højhed, Hans Vælde i Skyerne, frygtelig er Gud i sin Helligdom, Israels Gud; han giver Folket Styrke og Kraft. Lovet være Gud!

< Zaburi 68 >