< Zaburi 68 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Mungu na ainuke, watesi wake watawanyike, adui zake na wakimbie mbele zake.
大衛的詩歌,交與伶長。 願上帝興起,使他的仇敵四散, 叫那恨他的人從他面前逃跑。
2 Kama vile moshi upeperushwavyo na upepo, vivyo hivyo uwapeperushe mbali, kama vile nta iyeyukavyo kwenye moto, vivyo hivyo waovu na waangamie mbele za Mungu.
他們被驅逐,如煙被風吹散; 惡人見上帝之面而消滅,如蠟被火鎔化。
3 Bali wenye haki na wafurahi, washangilie mbele za Mungu, wafurahi na kushangilia.
惟有義人必然歡喜, 在上帝面前高興快樂。
4 Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake, mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu: jina lake ni Bwana, furahini mbele zake.
你們當向上帝唱詩,歌頌他的名; 為那坐車行過曠野的修平大路。 他的名是耶和華, 要在他面前歡樂!
5 Baba wa yatima, mtetezi wa wajane, ni Mungu katika makao yake matakatifu.
上帝在他的聖所作孤兒的父, 作寡婦的伸冤者。
6 Mungu huwaweka wapweke katika jamaa, huwaongoza wafungwa wakiimba, bali waasi huishi katika nchi kame.
上帝叫孤獨的有家, 使被囚的出來享福; 惟有悖逆的住在乾燥之地。
7 Ee Mungu, ulipowatangulia watu wako, ulipopita nyikani,
上帝啊,你曾在你百姓前頭出來, 在曠野行走。 (細拉)
8 dunia ilitikisika, mbingu zikanyesha mvua, mbele za Mungu, Yule wa Sinai, mbele za Mungu, Mungu wa Israeli.
那時,地見上帝的面而震動,天也落雨; 西奈山見以色列上帝的面也震動。
9 Ee Mungu, ulinyesha mvua nyingi na kuiburudisha ardhi iliyokuwa imechoka.
上帝啊,你降下大雨; 你產業以色列疲乏的時候,你使他堅固。
10 Ee Mungu, watu wako waliishi huko, nawe kwa wingi wa utajiri wako uliwapa maskini mahitaji yao.
你的會眾住在其中; 上帝啊,你的恩惠是為困苦人預備的。
11 Bwana alitangaza neno, waliolitangaza neno hilo walikuwa kundi kubwa:
主發命令, 傳好信息的婦女成了大群。
12 “Wafalme na majeshi walikimbia upesi, watu waliobaki kambini waligawana nyara.
統兵的君王逃跑了,逃跑了; 在家等候的婦女分受所奪的。
13 Hata ulalapo katikati ya mioto ya kambini, mabawa ya njiwa wangu yamefunikwa kwa fedha, manyoya yake kwa dhahabu ingʼaayo.”
你們安臥在羊圈的時候, 好像鴿子的翅膀鍍白銀,翎毛鍍黃金一般。
14 Wakati Mwenyezi alipowatawanya wafalme katika nchi, ilikuwa kama theluji iliyoanguka juu ya Salmoni.
全能者在境內趕散列王的時候, 勢如飄雪在撒們。
15 Milima ya Bashani ni milima iliyotukuka, milima ya Bashani ina vilele vilivyochongoka.
巴珊山是上帝的山; 巴珊山是多峰多嶺的山。
16 Enyi milima yenye vilele vilivyochongoka, kwa nini mnakazia macho kwa wivu, katika mlima Mungu anaochagua kutawala, ambako Bwana mwenyewe ataishi milele?
你們多峰多嶺的山哪, 為何斜看上帝所願居住的山? 耶和華必住這山,直到永遠!
17 Magari ya Mungu ni makumi ya maelfu, na maelfu ya maelfu; Bwana amekuja kutoka Sinai hadi katika patakatifu pake.
上帝的車輦累萬盈千; 主在其中,好像在西奈聖山一樣。
18 Ulipopanda juu, uliteka mateka, ukapokea vipawa kutoka kwa wanadamu, hata kutoka kwa wale walioasi, ili wewe, Ee Bwana Mungu, upate kuishi huko.
你已經升上高天,擄掠仇敵; 你在人間,就是在悖逆的人間,受了供獻, 叫耶和華上帝可以與他們同住。
19 Sifa apewe Bwana, Mungu Mwokozi wetu, ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu.
天天背負我們重擔的主, 就是拯救我們的上帝, 是應當稱頌的! (細拉)
20 Mungu wetu ni Mungu aokoaye, Bwana Mwenyezi hutuokoa na kifo.
上帝是為我們施行諸般救恩的上帝; 人能脫離死亡是在乎主耶和華。
21 Hakika Mungu ataponda vichwa vya adui zake, vichwa vya hao waendao katika njia za dhambi.
但上帝要打破他仇敵的頭, 就是那常犯罪之人的髮頂。
22 Bwana alisema, “Nitawarudisha kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari,
主說:我要使眾民從巴珊而歸, 使他們從深海而回,
23 ili uweze kuchovya miguu yako katika damu ya adui zako, huku ndimi za mbwa wako zikiwa na fungu lake.”
使你打碎仇敵,你的腳踹在血中, 使你狗的舌頭從其中得分。
24 Ee Mungu, maandamano yako yameonekana, maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, yakielekea patakatifu pake.
上帝啊,你是我的上帝,我的王; 人已經看見你行走,進入聖所。
25 Mbele wako waimbaji, baada yao wapiga vinanda, pamoja nao wako wanawali wakipiga matari.
歌唱的行在前,作樂的隨在後, 都在擊鼓的童女中間。
26 Msifuni Mungu katika kusanyiko kubwa, msifuni Bwana katika kusanyiko la Israeli.
從以色列源頭而來的, 當在各會中稱頌主上帝!
27 Liko kabila dogo la Benyamini likiwaongoza, wakifuatwa na kundi kubwa la watawala wa Yuda, hatimaye watawala wa Zabuloni na Naftali.
在那裏,有統管他們的小便雅憫, 有猶大的首領和他們的群眾, 有西布倫的首領, 有拿弗他利的首領。
28 Ee Mungu, amuru uwezo wako, Ee Mungu tuonyeshe nguvu zako, kama ulivyofanya hapo awali.
以色列的能力是上帝所賜的; 上帝啊,求你堅固你為我們所成全的事!
29 Kwa sababu ya Hekalu lako Yerusalemu wafalme watakuletea zawadi.
因你耶路撒冷的殿, 列王必帶貢物獻給你。
30 Mkemee mnyama aliyeko kwenye manyasi, kundi la mafahali katikati ya ndama za mataifa. Na walete minara ya madini ya fedha wakinyenyekea. Tawanya mataifa yapendayo vita.
求你叱喝蘆葦中的野獸和群公牛, 並列邦中的牛犢。 把銀塊踹在腳下; 上帝已經趕散好爭戰的列邦。
31 Wajumbe watakuja kutoka Misri, Kushi atajisalimisha kwa Mungu.
埃及的公侯要出來朝見上帝; 古實人要急忙舉手 禱告。
32 Mwimbieni Mungu, enyi falme za dunia, mwimbieni Bwana sifa,
世上的列國啊, 你們要向上帝歌唱; 願你們歌頌主!
33 mwimbieni sifa yeye apandaye mbingu za kale zilizo juu, yeye angurumaye kwa sauti kuu.
歌頌那自古駕行在諸天以上的主! 他發出聲音,是極大的聲音。
34 Tangazeni uwezo wa Mungu, ambaye fahari yake iko juu ya Israeli, ambaye uwezo wake uko katika anga.
你們要將能力歸給上帝。 他的威榮在以色列之上; 他的能力是在穹蒼。
35 Ee Mungu, wewe unatisha katika mahali patakatifu pako, Mungu wa Israeli huwapa watu wake uwezo na nguvu. Mungu Asifiwe!
上帝啊,你從聖所顯為可畏; 以色列的上帝是那將力量權能賜給他百姓的。 上帝是應當稱頌的!