< Zaburi 67 >

1 Kwa mwimbishaji. Na ala za nyuzi za muziki. Zaburi. Wimbo. Mungu aturehemu na kutubariki, na kutuangazia nuru za uso wake,
Mungu atuhurumie sisi na kutubariki na kufanya nuru ya uso wake ituangazie (Selah)
2 ili njia zako zijulikane duniani, wokovu wako katikati ya mataifa yote.
ili kwamba njia zako zijulikane nchi yote, wokovu wako kati ya mataifa yote.
3 Ee Mungu, mataifa na wakusifu, mataifa yote na wakusifu.
Watu wakusifu wewe, Mungu; watu wote wakusifu wewe.
4 Mataifa yote wafurahi na kuimba kwa shangwe, kwa kuwa unatawala watu kwa haki na kuongoza mataifa ya dunia.
Oh, mataifa wafurahi na na kuimba kwa furaha, maana utawahukumu watu kwa haki na kuwaongoza mataifa walioko duniani.
5 Ee Mungu, mataifa na wakusifu, mataifa yote na wakusifu.
Watu wakushukuru wewe, Mungu; watu wote wakusifu wewe.
6 Ndipo nchi itatoa mazao yake, naye Mungu, Mungu wetu, atatubariki.
Nchi imetoa mavuno yake na Mungu, Mungu wetu, ametubariki.
7 Mungu atatubariki na miisho yote ya dunia itamcha yeye.
Mungu ametubariki sisi, na miisho yote ya dunia itamuheshimu yeye.

< Zaburi 67 >