< Zaburi 65 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Ee Mungu, sifa zakungojea katika Sayuni; kwako wewe nadhiri zetu zitatimizwa.
למנצח מזמור לדוד שיר ב לך דמיה תהלה אלהים בציון ולך ישלם-נדר
2 Ewe usikiaye maombi, kwako wewe watu wote watakuja.
שמע תפלה-- עדיך כל-בשר יבאו
3 Tulipokuwa tumefunikwa kabisa na dhambi, wewe ulisamehe makosa yetu.
דברי עונת גברו מני פשעינו אתה תכפרם
4 Heri wale uliowachagua na kuwaleta karibu ili waishi katika nyua zako! Tunashibishwa kwa mema ya nyumba yako, mema ya Hekalu lako takatifu.
אשרי תבחר ותקרב-- ישכן חצריך נשבעה בטוב ביתך קדש היכלך
5 Unatujibu kwa matendo ya kushangaza ya haki, Ee Mungu Mwokozi wetu, tumaini la miisho yote ya duniani na la bahari zilizo mbali sana,
נוראות בצדק תעננו-- אלהי ישענו מבטח כל-קצוי-ארץ וים רחקים
6 uliyeumba milima kwa uwezo wako, ukiwa umejivika nguvu,
מכין הרים בכחו נאזר בגבורה
7 uliyenyamazisha dhoruba za bahari, ngurumo za mawimbi yake, na ghasia za mataifa.
משביח שאון ימים--שאון גליהם והמון לאמים
8 Wale wanaoishi mbali sana wanaogopa maajabu yako, kule asubuhi ipambazukiapo na kule jioni inakofifilia umeziita nyimbo za furaha.
וייראו ישבי קצות--מאותתיך מוצאי בקר וערב תרנין
9 Waitunza nchi na kuinyeshea, waitajirisha kwa wingi. Vijito vya Mungu vimejaa maji ili kuwapa watu nafaka, kwa maana wewe umeviamuru.
פקדת הארץ ותשקקה רבת תעשרנה-- פלג אלהים מלא מים תכין דגנם כי-כן תכינה
10 Umeilowesha mifereji yake na kusawazisha kingo zake; umeilainisha kwa manyunyu na kuibariki mimea yake.
תלמיה רוה נחת גדודה ברביבים תמגגנה צמחה תברך
11 Umeuvika mwaka taji ya baraka, magari yako yanafurika kwa wingi.
עטרת שנת טובתך ומעגליך ירעפון דשן
12 Mbuga za majani za jangwani umezineemesha; vilima vimevikwa furaha.
ירעפו נאות מדבר וגיל גבעות תחגרנה
13 Penye nyanda za malisho pamejaa makundi ya wanyama, na mabonde yamepambwa kwa mavuno; vyote vinashangilia kwa furaha na kuimba.
לבשו כרים הצאן-- ועמקים יעטפו-בר יתרועעו אף-ישירו

< Zaburi 65 >