< Zaburi 64 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, unisikie ninapoeleza lalamiko langu, uyahifadhi maisha yangu kutokana na vitisho vya adui.
Al Músico principal: Salmo de David. ESCUCHA, oh Dios, mi voz en mi oración: guarda mi vida del miedo del enemigo.
2 Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu, kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.
Escóndeme del secreto consejo de los malignos; de la conspiración de los que obran iniquidad:
3 Wananoa ndimi zao kama panga na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.
Que amolaron su lengua como cuchillo, [y] armaron [por] su saeta palabra amarga;
4 Hurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia, humrushia ghafula bila woga.
Para asaetear á escondidas al íntegro: de improviso lo asaetean, y no temen.
5 Kila mmoja humtia moyo mwenzake katika mipango mibaya; huzungumza juu ya kuficha mitego yao, nao husema, “Ni nani ataiona?”
Obstinados en su inicuo designio, tratan de esconder los lazos, [y] dicen: ¿Quién los ha de ver?
6 Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema, “Tumebuni mpango mkamilifu!” Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.
Inquieren iniquidades, hacen una investigación exacta; y el íntimo pensamiento de cada uno [de ellos], así como el corazón, [es] profundo.
7 Bali Mungu atawapiga kwa mishale, nao ghafula wataangushwa.
Mas Dios los herirá con saeta; de repente serán sus plagas.
8 Atageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao na kuwaleta kwenye maangamizi; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao kwa dharau.
Y harán caer sobre sí sus mismas lenguas: se espantarán todos los que los vieren.
9 Wanadamu wote wataogopa, watatangaza kazi za Mungu na kutafakari yale aliyoyatenda.
Y temerán todos los hombres, y anunciarán la obra de Dios, y entenderán su hecho.
10 Wenye haki na wafurahi katika Bwana, na wakimbilie kwake; wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!
Alegraráse el justo en Jehová, y confiaráse en él; y se gloriarán todos los rectos de corazón.

< Zaburi 64 >