< Zaburi 64 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, unisikie ninapoeleza lalamiko langu, uyahifadhi maisha yangu kutokana na vitisho vya adui.
O Dios, denggem ti timekko, denggem daytoy ararawko; annadam daytoy biagko iti panagbutengko kadagiti kabusorko.
2 Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu, kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.
Ilimmengnak iti nalimed a panagplano dagiti managdakdakes, manipud iti ringgor dagiti managbasol.
3 Wananoa ndimi zao kama panga na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.
Pinatademda dagiti dilada a kasla kampilan; dagiti napapait a sasaoda, kasla pana nga imbiatda
4 Hurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia, humrushia ghafula bila woga.
tapno mapanada ti awan basbasolna manipud iti nalimed a lugar; kellaat a panaenda isuna ket awan pagbutnganda.
5 Kila mmoja humtia moyo mwenzake katika mipango mibaya; huzungumza juu ya kuficha mitego yao, nao husema, “Ni nani ataiona?”
Allukoyenda dagiti babbagida iti dakes a panggep; agtutulagda iti nalimed tapno mangisagana kadagiti palab-og; kunada, “Siasino ngay ti makakita kadatayo?”
6 Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema, “Tumebuni mpango mkamilifu!” Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.
Agaramidda kadagiti dakes a panggep; “Nalpastayon,” kunada, “ti naannad a plano.” Nauneg ti kaunggan a panunot ken puso ti tao.
7 Bali Mungu atawapiga kwa mishale, nao ghafula wataangushwa.
Ngem panaen ida ti Dios; ket kellaat a masugatanda babaen kadagiti panana.
8 Atageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao na kuwaleta kwenye maangamizi; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao kwa dharau.
Maitibkoldanto, agsipud ta maibusor kadakuada dagiti dilada; agwingiwingto amin dagiti makakita kadakuada.
9 Wanadamu wote wataogopa, watatangaza kazi za Mungu na kutafakari yale aliyoyatenda.
Agbutengto dagiti amin a tattao ket ipadamagdanto dagiti inaramid ti Dios. Sisisiribdanto a mangpanunot iti inaramidna.
10 Wenye haki na wafurahi katika Bwana, na wakimbilie kwake; wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!
Agragsakto dagiti nalinteg gapu iti inaramid ni Yahweh ken agkamangdanto kenkuana; amin dagiti naimbag, ipannakkeldanto isuna.

< Zaburi 64 >