< Zaburi 64 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, unisikie ninapoeleza lalamiko langu, uyahifadhi maisha yangu kutokana na vitisho vya adui.
Dem Sangmeister. Ein Psalm Davids. Höre meine Stimme, Gott, in meiner Klage, bewahre mein Leben vor des Feindes Schauer.
2 Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu, kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.
Verbirg mich vor der Bösen Rotte, vor dem Gedränge derer, die Unrecht tun;
3 Wananoa ndimi zao kama panga na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.
Die ihre Zunge schärfen wie ein Schwert, die mit ihren Pfeilen zielen, mit bitterem Wort.
4 Hurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia, humrushia ghafula bila woga.
Die im Verborgenen schießen auf den Untadeligen; plötzlich schießen sie und fürchten sich nicht.
5 Kila mmoja humtia moyo mwenzake katika mipango mibaya; huzungumza juu ya kuficha mitego yao, nao husema, “Ni nani ataiona?”
Sie machen fest für sich die böse Sache, erzählen, wie sie hehlings Fallstricke legen; sie sagen: Wer sieht sie?
6 Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema, “Tumebuni mpango mkamilifu!” Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.
Sie erforschen Verkehrtes: Wir sind fertig, der Plan ist wohl überlegt; und das Innere des Mannes und das Herz sind tief.
7 Bali Mungu atawapiga kwa mishale, nao ghafula wataangushwa.
Aber Gott schießt sie mit einem Pfeil; plötzlich kommen ihre Schläge.
8 Atageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao na kuwaleta kwenye maangamizi; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao kwa dharau.
Und sie machen, daß sie straucheln; ihre Zunge ist wider sie; sie entfliehen, ein jeder, der sie sieht.
9 Wanadamu wote wataogopa, watatangaza kazi za Mungu na kutafakari yale aliyoyatenda.
Und alle Menschen fürchten sich und sagen an Gottes Werk und verstehen, was Er getan hat.
10 Wenye haki na wafurahi katika Bwana, na wakimbilie kwake; wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!
Der Gerechte ist fröhlich in Jehovah und verläßt sich auf Ihn, und es rühmen sich alle, die geraden Herzens sind.

< Zaburi 64 >