< Zaburi 64 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, unisikie ninapoeleza lalamiko langu, uyahifadhi maisha yangu kutokana na vitisho vya adui.
O Dieu, écoute ma voix quand je parle; garantis ma vie contre l'ennemi qui m'épouvante!
2 Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu, kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.
Mets-moi à couvert du complot des méchants, du tumulte des ouvriers d'iniquité;
3 Wananoa ndimi zao kama panga na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.
Qui aiguisent leur langue comme une épée, qui ajustent comme une flèche leur parole amère,
4 Hurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia, humrushia ghafula bila woga.
Pour tirer en secret sur l'innocent; ils tirent soudain contre lui, et n'ont point de crainte.
5 Kila mmoja humtia moyo mwenzake katika mipango mibaya; huzungumza juu ya kuficha mitego yao, nao husema, “Ni nani ataiona?”
Ils s'affermissent dans un mauvais dessein; ils ne parlent que de cacher des pièges; ils disent: Qui le verra?
6 Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema, “Tumebuni mpango mkamilifu!” Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.
Ils inventent des fraudes: Nous voilà prêts; le plan est formé! Et leur pensée secrète, le cœur de chacun est un abîme.
7 Bali Mungu atawapiga kwa mishale, nao ghafula wataangushwa.
Mais Dieu leur lance une flèche; soudain les voilà frappés.
8 Atageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao na kuwaleta kwenye maangamizi; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao kwa dharau.
Ceux que leur langue attaquait, les ont renversés; tous ceux qui les voient hochent la tête.
9 Wanadamu wote wataogopa, watatangaza kazi za Mungu na kutafakari yale aliyoyatenda.
Les hommes sont tous saisis de crainte; ils racontent l'œuvre de Dieu, et considèrent ce qu'il a fait.
10 Wenye haki na wafurahi katika Bwana, na wakimbilie kwake; wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!
Le juste se réjouira en l'Éternel, et se retirera vers lui; tous ceux qui ont le cœur droit s'en glorifieront.

< Zaburi 64 >