< Zaburi 64 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, unisikie ninapoeleza lalamiko langu, uyahifadhi maisha yangu kutokana na vitisho vya adui.
To the Overseer. — A Psalm of David. Hear, O God, my voice, in my (meditation) From the fear of an enemy Thou keepest my life,
2 Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu, kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.
Hidest me from the secret counsel of evil doers, From the tumult of workers of iniquity.
3 Wananoa ndimi zao kama panga na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.
Who sharpened as a sword their tongue, They directed their arrow — a bitter word.
4 Hurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia, humrushia ghafula bila woga.
To shoot in secret places the perfect, Suddenly they shoot him, and fear not.
5 Kila mmoja humtia moyo mwenzake katika mipango mibaya; huzungumza juu ya kuficha mitego yao, nao husema, “Ni nani ataiona?”
They strengthen for themselves an evil thing, They recount of the hiding of snares, They have said, 'Who doth look at it?'
6 Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema, “Tumebuni mpango mkamilifu!” Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.
They search out perverse things, 'We perfected a searching search,' And the inward part of man, and the heart [are] deep.
7 Bali Mungu atawapiga kwa mishale, nao ghafula wataangushwa.
And God doth shoot them [with] an arrow, Sudden have been their wounds,
8 Atageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao na kuwaleta kwenye maangamizi; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao kwa dharau.
And they cause him to stumble, Against them [is] their own tongue, Every looker on them fleeth away.
9 Wanadamu wote wataogopa, watatangaza kazi za Mungu na kutafakari yale aliyoyatenda.
And all men fear, and declare the work of God, And His deed they have considered wisely.
10 Wenye haki na wafurahi katika Bwana, na wakimbilie kwake; wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!
The righteous doth rejoice in Jehovah, And hath trusted in Him, And boast themselves do all the upright of heart!

< Zaburi 64 >