< Zaburi 64 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, unisikie ninapoeleza lalamiko langu, uyahifadhi maisha yangu kutokana na vitisho vya adui.
God, listen to me as I tell you the things that I am worried about. I am afraid of my enemies; so save/rescue me from them.
2 Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu, kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.
Protect me from what wicked men are planning to do to me; protect me from that gang of men who do what is evil.
3 Wananoa ndimi zao kama panga na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.
The hostile things they say [MTY] are like [SIM] [sharp] swords; their cruel words are like [SIM] arrows.
4 Hurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia, humrushia ghafula bila woga.
Without being afraid, they [lie about people and slander people] who have not done what is wrong, like someone who suddenly jumps up from where he is hiding and shoots [arrows] at his enemy [MET].
5 Kila mmoja humtia moyo mwenzake katika mipango mibaya; huzungumza juu ya kuficha mitego yao, nao husema, “Ni nani ataiona?”
They encourage each other about doing the evil things that they are planning to do; they talk [with each other] about where they can set traps to catch people, and they think, “No one [RHQ] will see what we are doing,
6 Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema, “Tumebuni mpango mkamilifu!” Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.
because we have planned very well the crime that we are going to commit!” No one can fully understand what people can think and plan!
7 Bali Mungu atawapiga kwa mishale, nao ghafula wataangushwa.
But [it will be as though] God will shoot his arrows at them, and suddenly they will be wounded.
8 Atageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao na kuwaleta kwenye maangamizi; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao kwa dharau.
Because of what they say [MTY], he will get rid of them, and then everyone who sees [what has happened to] them will shake their heads [to ridicule them].
9 Wanadamu wote wataogopa, watatangaza kazi za Mungu na kutafakari yale aliyoyatenda.
And then everyone will be afraid [to sin because of what might happen to them, also]; they will tell others what God has done, and they themselves will think much about it.
10 Wenye haki na wafurahi katika Bwana, na wakimbilie kwake; wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!
Righteous people should rejoice because of what Yahweh [has done]; they should go to him to (find protection/be safe); and all those who are godly will praise him.