< Zaburi 64 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, unisikie ninapoeleza lalamiko langu, uyahifadhi maisha yangu kutokana na vitisho vya adui.
To the choirmaster a psalm of David. Hear O God voice my in complaint my from dread of an enemy you will preserve life my.
2 Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu, kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.
You will hide me from [the] secret counsel of evil-doers from [the] unrest of [those who] do wickedness.
3 Wananoa ndimi zao kama panga na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.
Who they sharpen like sword tongue their they bend arrow their a word bitter.
4 Hurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia, humrushia ghafula bila woga.
To shoot in secret places [the] blameless suddenly they shoot at him and not they are afraid.
5 Kila mmoja humtia moyo mwenzake katika mipango mibaya; huzungumza juu ya kuficha mitego yao, nao husema, “Ni nani ataiona?”
They strengthen for themselves - a matter evil they speak to hide snares they say who? will he see them.
6 Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema, “Tumebuni mpango mkamilifu!” Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.
They plot injustice we have finished a plot plotted and [the] inner being of a person and [the] heart [is] deep.
7 Bali Mungu atawapiga kwa mishale, nao ghafula wataangushwa.
And he shot at them God an arrow suddenly they will be wounds their.
8 Atageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao na kuwaleta kwenye maangamizi; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao kwa dharau.
And they caused to stumble him [is] on them tongue their they will shudder every [one who] looks on them.
9 Wanadamu wote wataogopa, watatangaza kazi za Mungu na kutafakari yale aliyoyatenda.
And they were afraid all humankind and they declared [the] deed[s] of God and work his they will consider.
10 Wenye haki na wafurahi katika Bwana, na wakimbilie kwake; wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!
Let him rejoice [the] righteous in Yahweh and he will take refuge in him and let them boast all [people] upright of heart.