< Zaburi 64 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, unisikie ninapoeleza lalamiko langu, uyahifadhi maisha yangu kutokana na vitisho vya adui.
For the leader. A psalm of David. Hear, O my God, the voice of my lament: guard my life from the dread of the foe.
2 Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu, kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.
Hide me from villains who secretly plot, from the blustering throng of the workers of evil,
3 Wananoa ndimi zao kama panga na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.
who have sharpened their tongue like a sword, and aimed bitter words like arrows,
4 Hurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia, humrushia ghafula bila woga.
which from ambush they launch at the blameless, shooting swiftly and unafraid.
5 Kila mmoja humtia moyo mwenzake katika mipango mibaya; huzungumza juu ya kuficha mitego yao, nao husema, “Ni nani ataiona?”
They strengthen their wicked purpose, they tell of the snares they have hidden, they say to themselves, “Who can see?”
6 Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema, “Tumebuni mpango mkamilifu!” Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.
They think out their crimes full cunningly hidden deep in their crafty hearts.
7 Bali Mungu atawapiga kwa mishale, nao ghafula wataangushwa.
But God with his arrow will shoot them, swiftly shall they be smitten.
8 Atageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao na kuwaleta kwenye maangamizi; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao kwa dharau.
For their tongue he will bring them to ruin, all will shudder with horror at the sight of them.
9 Wanadamu wote wataogopa, watatangaza kazi za Mungu na kutafakari yale aliyoyatenda.
Then every person, touched to awe, as they ponder what God has wrought, will tell the tale of his deeds.
10 Wenye haki na wafurahi katika Bwana, na wakimbilie kwake; wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!
In the Lord shall the righteous rejoice, in him shall they take refuge; and all the true-hearted shall glory.