< Zaburi 64 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, unisikie ninapoeleza lalamiko langu, uyahifadhi maisha yangu kutokana na vitisho vya adui.
To him that excelleth. A Psalme of David. Heare my voyce, O God, in my prayer: preserue my life from feare of the enemie.
2 Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu, kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.
Hide me from the conspiracie of the wicked, and from the rage of the workers of iniquitie.
3 Wananoa ndimi zao kama panga na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.
Which haue whette their tongue like a sword, and shot for their arrowes bitter wordes.
4 Hurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia, humrushia ghafula bila woga.
To shoote at the vpright in secrete: they shoote at him suddenly, and feare not.
5 Kila mmoja humtia moyo mwenzake katika mipango mibaya; huzungumza juu ya kuficha mitego yao, nao husema, “Ni nani ataiona?”
They encourage themselues in a wicked purpose: they commune together to lay snares priuilie, and say, Who shall see them?
6 Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema, “Tumebuni mpango mkamilifu!” Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.
They haue sought out iniquities, and haue accomplished that which they sought out, euen euery one his secret thoughtes, and the depth of his heart.
7 Bali Mungu atawapiga kwa mishale, nao ghafula wataangushwa.
But God will shoote an arrowe at them suddenly: their strokes shalbe at once.
8 Atageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao na kuwaleta kwenye maangamizi; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao kwa dharau.
They shall cause their owne tongue to fall vpon them: and whosoeuer shall see them, shall flee away.
9 Wanadamu wote wataogopa, watatangaza kazi za Mungu na kutafakari yale aliyoyatenda.
And all men shall see it, and declare the worke of God, and they shall vnderstand, what he hath wrought.
10 Wenye haki na wafurahi katika Bwana, na wakimbilie kwake; wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!
But the righteous shall be glad in the Lord, and trust in him: and all that are vpright of heart, shall reioyce.