< Zaburi 64 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, unisikie ninapoeleza lalamiko langu, uyahifadhi maisha yangu kutokana na vitisho vya adui.
For the music director. A psalm of David. God, please listen to my complaint. Protect me because my enemies scare me.
2 Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu, kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.
Shelter me from the plots of the wicked, from this evil mob.
3 Wananoa ndimi zao kama panga na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.
What they say cuts like swords; they fire off poisonous words like arrows.
4 Hurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia, humrushia ghafula bila woga.
They shoot from their hiding places at innocent people—doing this without warning, not afraid of being caught.
5 Kila mmoja humtia moyo mwenzake katika mipango mibaya; huzungumza juu ya kuficha mitego yao, nao husema, “Ni nani ataiona?”
They encourage one another to do evil, planning how to secretly trap people, telling themselves, “Nobody will notice.”
6 Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema, “Tumebuni mpango mkamilifu!” Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.
They plot wicked things. “What a great plan we've created!” they say. There are no limits to the depths to which human minds and thoughts can sink.
7 Bali Mungu atawapiga kwa mishale, nao ghafula wataangushwa.
But God will shoot them with arrows; all of a sudden they will be wounded.
8 Atageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao na kuwaleta kwenye maangamizi; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao kwa dharau.
What they themselves say will trip them up; people who see them will mock them, shaking their heads at them.
9 Wanadamu wote wataogopa, watatangaza kazi za Mungu na kutafakari yale aliyoyatenda.
Then everyone will be frightened. They will say that this is the work of God, and they will think about what he has done.
10 Wenye haki na wafurahi katika Bwana, na wakimbilie kwake; wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!
Those who are right with the Lord will be happy in him, they will go to him for protection. Those who live right will praise him.