< Zaburi 64 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, unisikie ninapoeleza lalamiko langu, uyahifadhi maisha yangu kutokana na vitisho vya adui.
Unto the end, a psalm for David. Hear, O God, my prayer, when I make supplication to thee: deliver my soul from the fear of the enemy.
2 Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu, kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.
Thou hast protected me from the assembly of the malignant; from the multitude of the workers of iniquity.
3 Wananoa ndimi zao kama panga na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.
For they have whetted their tongues like a sword; they have bent their bow a bitter thing,
4 Hurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia, humrushia ghafula bila woga.
To shoot in secret the undefiled.
5 Kila mmoja humtia moyo mwenzake katika mipango mibaya; huzungumza juu ya kuficha mitego yao, nao husema, “Ni nani ataiona?”
They will shoot at him on a sudden, and will not fear: they are resolute in wickedness. They have talked of hiding snares; they have said: Who shall see them?
6 Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema, “Tumebuni mpango mkamilifu!” Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.
They have searched after iniquities: they have failed in their search. Man shall come to a deep heart:
7 Bali Mungu atawapiga kwa mishale, nao ghafula wataangushwa.
And God shall be exalted. The arrows of children are their wounds:
8 Atageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao na kuwaleta kwenye maangamizi; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao kwa dharau.
And their tongues against them are made weak. All that saw them were troubled;
9 Wanadamu wote wataogopa, watatangaza kazi za Mungu na kutafakari yale aliyoyatenda.
And every man was afraid. And they declared the works of God: and understood his doings.
10 Wenye haki na wafurahi katika Bwana, na wakimbilie kwake; wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!
The just shall rejoice in the Lord, and shall hope in him: and all the upright in heart shall be praised.

< Zaburi 64 >