< Zaburi 63 >

1 Zaburi ya Daudi. Wakati alipokuwa katika Jangwa la Yuda. Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, nakutafuta kwa moyo wote; nafsi yangu inakuonea kiu, mwili wangu unakuonea wewe shauku, katika nchi kame na iliyochoka mahali ambapo hapana maji.
Oh Dios, tú eres mi Dios; de madrugada te buscaré: mi alma está seca por necesidad de ti, mi carne se desperdicia con deseo por ti, como una tierra seca y ardiente donde no hay agua;
2 Nimekuona katika mahali patakatifu na kuuona uwezo wako na utukufu wako.
Para ver tu poder y tu gloria, como te he visto en el lugar santo.
3 Kwa sababu upendo wako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakuadhimisha.
Porque tu misericordia es mejor que la vida, mis labios te darán alabanza.
4 Nitakusifu siku zote za maisha yangu, na kwa jina lako nitainua mikono yangu.
Así que continuaré bendiciéndote toda mi vida, levantando mis manos en tu nombre.
5 Nafsi yangu itatoshelezwa kama kwa wingi wa vyakula; kwa midomo iimbayo kinywa changu kitakusifu wewe.
Mi alma será consolada, como con buena comida; y mi boca te dará alabanza con canciones de alegría;
6 Kitandani mwangu ninakukumbuka wewe, ninawaza juu yako makesha yote ya usiku.
Cuando el recuerdo de ti viene a mí en mi cama, y ​​cuando pienso en ti por la noche.
7 Kwa sababu wewe ndiwe msaada wangu, chini ya uvuli wa mbawa zako naimba.
Porque has sido mi ayuda, tendré gozo a la sombra de tus alas.
8 Nafsi yangu inaambatana nawe, mkono wako wa kuume hunishika.
Mi alma se mantiene siempre cerca de ti: tu diestra es mi apoyo.
9 Wale wanaotafuta uhai wangu wataharibiwa, watakwenda chini kwenye vilindi vya dunia.
Pero aquellos cuyo deseo es la destrucción de mi alma bajará a las partes más bajas de la tierra.
10 Watatolewa wafe kwa upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
Serán cortados por la espada; serán alimento para zorros.
11 Bali mfalme atafurahi katika Mungu, wale wote waapao kwa jina la Mungu watamsifu, bali vinywa vya waongo vitanyamazishwa.
Pero el rey tendrá gozo en Dios; todos los que juran por él tendrán motivos de orgullo; pero la boca falsa se detendrá.

< Zaburi 63 >