< Zaburi 63 >
1 Zaburi ya Daudi. Wakati alipokuwa katika Jangwa la Yuda. Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, nakutafuta kwa moyo wote; nafsi yangu inakuonea kiu, mwili wangu unakuonea wewe shauku, katika nchi kame na iliyochoka mahali ambapo hapana maji.
Salmo de David, estando en el desierto de Judá. DIOS, Dios mío eres tú: levantaréme á ti de mañana: mi alma tiene sed de ti, mi carne te desea, en tierra de sequedad y transida sin aguas;
2 Nimekuona katika mahali patakatifu na kuuona uwezo wako na utukufu wako.
Para ver tu fortaleza y tu gloria, así como te he mirado en el santuario.
3 Kwa sababu upendo wako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakuadhimisha.
Porque mejor es tu misericordia que la vida: mis labios te alabarán.
4 Nitakusifu siku zote za maisha yangu, na kwa jina lako nitainua mikono yangu.
Así te bendeciré en mi vida: en tu nombre alzaré mis manos.
5 Nafsi yangu itatoshelezwa kama kwa wingi wa vyakula; kwa midomo iimbayo kinywa changu kitakusifu wewe.
Como de meollo y de grosura será saciada mi alma; y con labios de júbilo te alabará mi boca,
6 Kitandani mwangu ninakukumbuka wewe, ninawaza juu yako makesha yote ya usiku.
Cuando me acordaré de ti en mi lecho, [cuando] meditaré de ti en las velas de la noche.
7 Kwa sababu wewe ndiwe msaada wangu, chini ya uvuli wa mbawa zako naimba.
Porque has sido mi socorro; y [así] en la sombra de tus alas me regocijaré.
8 Nafsi yangu inaambatana nawe, mkono wako wa kuume hunishika.
Está mi alma apegada á ti: tu diestra me ha sostenido.
9 Wale wanaotafuta uhai wangu wataharibiwa, watakwenda chini kwenye vilindi vya dunia.
Mas los que para destrucción buscaron mi alma, caerán en los sitios bajos de la tierra.
10 Watatolewa wafe kwa upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
Destruiránlos á filo de espada; serán porción de las zorras.
11 Bali mfalme atafurahi katika Mungu, wale wote waapao kwa jina la Mungu watamsifu, bali vinywa vya waongo vitanyamazishwa.
Empero el rey se alegrará en Dios; será alabado cualquiera que por él jura: porque la boca de los que hablan mentira, será cerrada.