< Zaburi 63 >
1 Zaburi ya Daudi. Wakati alipokuwa katika Jangwa la Yuda. Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, nakutafuta kwa moyo wote; nafsi yangu inakuonea kiu, mwili wangu unakuonea wewe shauku, katika nchi kame na iliyochoka mahali ambapo hapana maji.
Dios, Dios mío eres tú, a ti madrugaré: mi alma tuvo sed de ti, mi carne te desea en tierra de sequedad, y sequiosa sin aguas.
2 Nimekuona katika mahali patakatifu na kuuona uwezo wako na utukufu wako.
Así te miré en el santuario, para ver tu fortaleza y tu gloria.
3 Kwa sababu upendo wako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakuadhimisha.
Porque mejor es tu misericordia que la vida: mis labios te alabarán.
4 Nitakusifu siku zote za maisha yangu, na kwa jina lako nitainua mikono yangu.
Así te bendeciré en mi vida: en tu nombre alzaré mis manos.
5 Nafsi yangu itatoshelezwa kama kwa wingi wa vyakula; kwa midomo iimbayo kinywa changu kitakusifu wewe.
Como de meollo y de grosura será harta mi alma: y con labios de alegría te alabará mi boca,
6 Kitandani mwangu ninakukumbuka wewe, ninawaza juu yako makesha yote ya usiku.
Cuando me acordaré de ti en mis camas, cuando a las alboradas meditaré de ti;
7 Kwa sababu wewe ndiwe msaada wangu, chini ya uvuli wa mbawa zako naimba.
Porque has sido mi socorro: y en la sombra de tus alas me regocijaré.
8 Nafsi yangu inaambatana nawe, mkono wako wa kuume hunishika.
Mi alma se apegó a ti: tu diestra me ha sustentado.
9 Wale wanaotafuta uhai wangu wataharibiwa, watakwenda chini kwenye vilindi vya dunia.
Mas ellos para destrucción buscaron mi alma: descendieron en lo más bajo de la tierra.
10 Watatolewa wafe kwa upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
Matarlos han a filo de espada: porción de zorras serán.
11 Bali mfalme atafurahi katika Mungu, wale wote waapao kwa jina la Mungu watamsifu, bali vinywa vya waongo vitanyamazishwa.
Y el rey se alegrará en Dios, será alabado cualquiera que jura por él: porque la boca de los que hablan mentira, será cerrada.