< Zaburi 63 >

1 Zaburi ya Daudi. Wakati alipokuwa katika Jangwa la Yuda. Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, nakutafuta kwa moyo wote; nafsi yangu inakuonea kiu, mwili wangu unakuonea wewe shauku, katika nchi kame na iliyochoka mahali ambapo hapana maji.
Un salmo de David, cuando estaba en el desierto de Judá. Dios, tú eres mi Dios. Te buscaré con ahínco. Mi alma tiene sed de ti. Mi carne te anhela, en una tierra seca y cansada, donde no hay agua.
2 Nimekuona katika mahali patakatifu na kuuona uwezo wako na utukufu wako.
Así te he visto en el santuario, viendo tu poder y tu gloria.
3 Kwa sababu upendo wako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakuadhimisha.
Porque tu bondad amorosa es mejor que la vida, mis labios te alabarán.
4 Nitakusifu siku zote za maisha yangu, na kwa jina lako nitainua mikono yangu.
Así te bendeciré mientras viva. Levantaré mis manos en tu nombre.
5 Nafsi yangu itatoshelezwa kama kwa wingi wa vyakula; kwa midomo iimbayo kinywa changu kitakusifu wewe.
Mi alma se saciará como del más rico alimento. Mi boca te alabará con labios alegres,
6 Kitandani mwangu ninakukumbuka wewe, ninawaza juu yako makesha yote ya usiku.
cuando te recuerdo en mi cama, y pensar en ti en las guardias nocturnas.
7 Kwa sababu wewe ndiwe msaada wangu, chini ya uvuli wa mbawa zako naimba.
Porque tú has sido mi ayuda. Me alegraré a la sombra de tus alas.
8 Nafsi yangu inaambatana nawe, mkono wako wa kuume hunishika.
Mi alma permanece cerca de ti. Tu mano derecha me sostiene.
9 Wale wanaotafuta uhai wangu wataharibiwa, watakwenda chini kwenye vilindi vya dunia.
Pero los que buscan mi alma para destruirla irán a las partes bajas de la tierra.
10 Watatolewa wafe kwa upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
Serán entregados al poder de la espada. Serán comida para chacales.
11 Bali mfalme atafurahi katika Mungu, wale wote waapao kwa jina la Mungu watamsifu, bali vinywa vya waongo vitanyamazishwa.
Pero el rey se alegrará en Dios. Todos los que juran por él lo alabarán, porque la boca de los que hablan mentiras será silenciada.

< Zaburi 63 >