< Zaburi 63 >
1 Zaburi ya Daudi. Wakati alipokuwa katika Jangwa la Yuda. Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, nakutafuta kwa moyo wote; nafsi yangu inakuonea kiu, mwili wangu unakuonea wewe shauku, katika nchi kame na iliyochoka mahali ambapo hapana maji.
Un salmo de David, cuando estaba en el desierto de Judá. Dios, tú eres mi Dios y te busco de todo corazón. Mi ser entero te anhela y tiene sed de ti, en medio de esta tierra seca, árida y carente de aguas.
2 Nimekuona katika mahali patakatifu na kuuona uwezo wako na utukufu wako.
Te veo en el Templo. Contemplo tu poder y tu gloria.
3 Kwa sababu upendo wako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakuadhimisha.
Tu fidelidad y amor son mejores que la vida misma. Por ello te alabaré.
4 Nitakusifu siku zote za maisha yangu, na kwa jina lako nitainua mikono yangu.
Te agradeceré tanto como viva. Elevo mis manos hacia ti y celebro tu maravilloso carácter.
5 Nafsi yangu itatoshelezwa kama kwa wingi wa vyakula; kwa midomo iimbayo kinywa changu kitakusifu wewe.
Tú me satisfaces más que el mejor de los alimentos. Te alabaré con canciones alegres.
6 Kitandani mwangu ninakukumbuka wewe, ninawaza juu yako makesha yote ya usiku.
Paso la noche entera pensando en ti desde que me acuesto, meditando sobre ti.
7 Kwa sababu wewe ndiwe msaada wangu, chini ya uvuli wa mbawa zako naimba.
Porque eres quien me ayuda, canto feliz bajo tus alas.
8 Nafsi yangu inaambatana nawe, mkono wako wa kuume hunishika.
Me aferro a ti y tus fuertes brazos me levantan.
9 Wale wanaotafuta uhai wangu wataharibiwa, watakwenda chini kwenye vilindi vya dunia.
Los que tratan de destruirme irán a la tumba.
10 Watatolewa wafe kwa upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
Morirán a punta de espada y serán alimento para los chacales.
11 Bali mfalme atafurahi katika Mungu, wale wote waapao kwa jina la Mungu watamsifu, bali vinywa vya waongo vitanyamazishwa.
Pero el rey vivirá feliz por todo lo que Dios ha hecho. Todos los que siguen a Dios le alabarán, pero los que mienten serán silenciados.