< Zaburi 63 >
1 Zaburi ya Daudi. Wakati alipokuwa katika Jangwa la Yuda. Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, nakutafuta kwa moyo wote; nafsi yangu inakuonea kiu, mwili wangu unakuonea wewe shauku, katika nchi kame na iliyochoka mahali ambapo hapana maji.
Um salmo de David, quando ele estava no deserto de Judá. God, você é meu Deus. Vou procurá-lo com seriedade. Minha alma tem sede por você. Minha carne anseia por você, em uma terra seca e cansada, onde não há água.
2 Nimekuona katika mahali patakatifu na kuuona uwezo wako na utukufu wako.
Então, eu o vi no santuário, observando seu poder e sua glória.
3 Kwa sababu upendo wako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakuadhimisha.
Porque sua bondade amorosa é melhor que a vida, meus lábios vos louvarão.
4 Nitakusifu siku zote za maisha yangu, na kwa jina lako nitainua mikono yangu.
Portanto, eu o abençoarei enquanto eu viver. Levantarei minhas mãos em seu nome.
5 Nafsi yangu itatoshelezwa kama kwa wingi wa vyakula; kwa midomo iimbayo kinywa changu kitakusifu wewe.
Minha alma deve estar satisfeita como com os alimentos mais ricos. Minha boca vos louvará com lábios alegres,
6 Kitandani mwangu ninakukumbuka wewe, ninawaza juu yako makesha yote ya usiku.
quando me lembro de você na minha cama, e pensar em você nos relógios noturnos.
7 Kwa sababu wewe ndiwe msaada wangu, chini ya uvuli wa mbawa zako naimba.
Para você tem sido minha ajuda. Eu me regozijarei à sombra de suas asas.
8 Nafsi yangu inaambatana nawe, mkono wako wa kuume hunishika.
Minha alma permanece perto de você. Sua mão direita me segura para cima.
9 Wale wanaotafuta uhai wangu wataharibiwa, watakwenda chini kwenye vilindi vya dunia.
Mas aqueles que buscam minha alma para destruí-la devem ir para as partes mais baixas da terra.
10 Watatolewa wafe kwa upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
Eles serão entregues ao poder da espada. Devem ser comida de chacal.
11 Bali mfalme atafurahi katika Mungu, wale wote waapao kwa jina la Mungu watamsifu, bali vinywa vya waongo vitanyamazishwa.
Mas o rei se regozijará em Deus. Todos que jurarem por ele irão elogiá-lo, pois a boca daqueles que falam mentiras será silenciada.