< Zaburi 63 >
1 Zaburi ya Daudi. Wakati alipokuwa katika Jangwa la Yuda. Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, nakutafuta kwa moyo wote; nafsi yangu inakuonea kiu, mwili wangu unakuonea wewe shauku, katika nchi kame na iliyochoka mahali ambapo hapana maji.
Nzembo ya Davidi. Ayembaki yango tango azalaki kati na esobe ya Yuda. Oh Nzambe, ozali Nzambe na ngai; nazali koluka Yo, molimo na ngai ezali na posa na Yo, bomoi na ngai ezali na posa na Yo makasi, kati na mabele ekawuka mpe ezanga mayi.
2 Nimekuona katika mahali patakatifu na kuuona uwezo wako na utukufu wako.
Natalaki Yo kati na Esika ya bule mpo na komona makasi mpe nkembo na Yo.
3 Kwa sababu upendo wako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakuadhimisha.
Pamba te bolingo na Yo ezali malamu koleka bomoi, bibebu na ngai ekosanzola Yo.
4 Nitakusifu siku zote za maisha yangu, na kwa jina lako nitainua mikono yangu.
Boye, nakopambola Yo bomoi na ngai mobimba, nakotombola maboko na ngai mpo na lokumu ya Kombo na Yo.
5 Nafsi yangu itatoshelezwa kama kwa wingi wa vyakula; kwa midomo iimbayo kinywa changu kitakusifu wewe.
Nakotonda lokola moto oyo asili kolia misuni kitoko mpe mafuta; bibebu na ngai ekoganga na esengo mpe monoko na ngai ekokumisa Yo.
6 Kitandani mwangu ninakukumbuka wewe, ninawaza juu yako makesha yote ya usiku.
Soki nakanisi Yo na mbeto na ngai, nasambelaka Yo na butu;
7 Kwa sababu wewe ndiwe msaada wangu, chini ya uvuli wa mbawa zako naimba.
pamba te ozali lisungi mpo na ngai, mpe nagangaka na esengo wana nazali na se ya elili ya mapapu na Yo.
8 Nafsi yangu inaambatana nawe, mkono wako wa kuume hunishika.
Nakangami na Yo; loboko na Yo ya mobali esimbi ngai makasi.
9 Wale wanaotafuta uhai wangu wataharibiwa, watakwenda chini kwenye vilindi vya dunia.
Bato oyo balukaka koboma ngai bakozinda na mabele
10 Watatolewa wafe kwa upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
Bakoboma bango na mopanga mpe bakokoma bilei ya bambwa ya zamba.
11 Bali mfalme atafurahi katika Mungu, wale wote waapao kwa jina la Mungu watamsifu, bali vinywa vya waongo vitanyamazishwa.
Kasi mokonzi akosepela kati na Nzambe; moto nyonso oyo alapaka ndayi na Kombo ya Nzambe akomikumisa mpo na yango, pamba te minoko ya bakosi ekokangama.