< Zaburi 63 >
1 Zaburi ya Daudi. Wakati alipokuwa katika Jangwa la Yuda. Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, nakutafuta kwa moyo wote; nafsi yangu inakuonea kiu, mwili wangu unakuonea wewe shauku, katika nchi kame na iliyochoka mahali ambapo hapana maji.
Daavidin virsi, kun hän oli Juudan erämaassa. Jumala, sinä olet minun Jumalani, sinua minä etsin varhain; sinua minun sieluni janoaa, sinua halajaa minun ruumiini kuivassa ja nääntyvässä, vedettömässä maassa.
2 Nimekuona katika mahali patakatifu na kuuona uwezo wako na utukufu wako.
Niin minä katselin sinua pyhäkössä, nähdäkseni sinun voimasi ja kunniasi.
3 Kwa sababu upendo wako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakuadhimisha.
Sillä sinun armosi on parempi kuin elämä, minun huuleni ylistäkööt sinua.
4 Nitakusifu siku zote za maisha yangu, na kwa jina lako nitainua mikono yangu.
Niin minä kiitän sinua elinaikani, nostan käteni sinun nimeesi.
5 Nafsi yangu itatoshelezwa kama kwa wingi wa vyakula; kwa midomo iimbayo kinywa changu kitakusifu wewe.
Minun sieluni ravitaan niinkuin lihavuudella ja rasvalla, ja minun suuni ylistää sinua riemuitsevilla huulilla,
6 Kitandani mwangu ninakukumbuka wewe, ninawaza juu yako makesha yote ya usiku.
kun minä vuoteessani sinua muistan ja ajattelen sinua yön vartiohetkinä.
7 Kwa sababu wewe ndiwe msaada wangu, chini ya uvuli wa mbawa zako naimba.
Sillä sinä olet minun apuni, ja sinun siipiesi suojassa minä riemuitsen.
8 Nafsi yangu inaambatana nawe, mkono wako wa kuume hunishika.
Minun sieluni riippuu sinussa kiinni, sinun oikea kätesi tukee minua.
9 Wale wanaotafuta uhai wangu wataharibiwa, watakwenda chini kwenye vilindi vya dunia.
Mutta he etsivät minun henkeäni omaksi turmiokseen, he menevät maan syvyyksiin.
10 Watatolewa wafe kwa upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
Heidät annetaan miekalle alttiiksi, he joutuvat aavikkosutten osaksi.
11 Bali mfalme atafurahi katika Mungu, wale wote waapao kwa jina la Mungu watamsifu, bali vinywa vya waongo vitanyamazishwa.
Mutta kuningas on iloitseva Jumalassa; hän on jokaisen kerskaus, joka hänen kauttansa vannoo. Sillä valhettelijain suu tukitaan.