< Zaburi 63 >

1 Zaburi ya Daudi. Wakati alipokuwa katika Jangwa la Yuda. Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, nakutafuta kwa moyo wote; nafsi yangu inakuonea kiu, mwili wangu unakuonea wewe shauku, katika nchi kame na iliyochoka mahali ambapo hapana maji.
Een psalm van David, toen hij in de woestijn van Juda vertoefde. God, wat verlang ik naar U; mijn God, naar U dorst mijn ziel, Naar U smacht mijn lichaam als een dor en droog land naar het water.
2 Nimekuona katika mahali patakatifu na kuuona uwezo wako na utukufu wako.
Ik blik naar U op in uw heilige woning, Om uw macht en uw glorie te aanschouwen!
3 Kwa sababu upendo wako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakuadhimisha.
Ja, uw genade is kostelijker nog dan het leven: Daarom moeten mijn lippen U loven,
4 Nitakusifu siku zote za maisha yangu, na kwa jina lako nitainua mikono yangu.
En wil ik U al mijn dagen prijzen, Mijn handen opheffen in uw Naam.
5 Nafsi yangu itatoshelezwa kama kwa wingi wa vyakula; kwa midomo iimbayo kinywa changu kitakusifu wewe.
Gij verzadigt mij als met vet en met merg, En mijn mond juicht U toe met jubelende lippen;
6 Kitandani mwangu ninakukumbuka wewe, ninawaza juu yako makesha yote ya usiku.
Nog op mijn legerstede moet ik aan U denken, En in mijn nachtwaken over U peinzen.
7 Kwa sababu wewe ndiwe msaada wangu, chini ya uvuli wa mbawa zako naimba.
Want Gij zijt mijn Helper, Ik nestel in de schaduw uwer vleugelen;
8 Nafsi yangu inaambatana nawe, mkono wako wa kuume hunishika.
Mijn ziel klampt zich aan U vast, En uw rechterhand is mij een stut.
9 Wale wanaotafuta uhai wangu wataharibiwa, watakwenda chini kwenye vilindi vya dunia.
Maar zij, die mijn ondergang zoeken, Zullen in de diepten der aarde verzinken;
10 Watatolewa wafe kwa upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
Ze vallen ten prooi aan het zwaard, En worden een buit van de jakhalzen.
11 Bali mfalme atafurahi katika Mungu, wale wote waapao kwa jina la Mungu watamsifu, bali vinywa vya waongo vitanyamazishwa.
Doch de Koning zal zich verheugen in God, En wie Hem trouw zweert, zal juichen; Maar de mond van de leugenaars wordt gestopt!

< Zaburi 63 >