< Zaburi 61 >

1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za uimbaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, sikia kilio changu, usikilize maombi yangu.
O Dios, denggem ti asugko ken ipangagmo ti kararagko.
2 Kutoka miisho ya dunia ninakuita, ninaita huku moyo wangu unadhoofika; uniongoze kwenye mwamba ule ulio juu kuliko mimi.
Umawagak kenka manipud iti pagpatingaan ti daga no madagdagsenan ti pusok; iturongnak iti bato a nangatngato ngem siak.
3 Kwa kuwa umekuwa kimbilio langu, ngome imara dhidi ya adui.
Ta sika ti salaknibko, natibker a torre manipud kadagiti kabusor.
4 Natamani kukaa hemani mwako milele, na kukimbilia chini ya uvuli wa mbawa zako.
Agnanayonto nga agtalinaedak iti tabernakulom; agkamangak iti salukob dagiti payyakmo. (Selah)
5 Ee Mungu, kwa kuwa umesikia nadhiri zangu, umenipa urithi wa wale wanaoliogopa jina lako.
Ta nangngegmo O Dios dagiti sapatak; intedmo kaniak iti tawid nga ipaaymo koma kadagidiay a mangpadayaw iti naganmo.
6 Mwongezee mfalme siku za maisha yake, miaka yake kwa vizazi vingi.
Paatiddogem ti biag ti ari, agbalinto a kas kapaut dagiti henerasion ti tawenna.
7 Yeye na atawazwe kwenye kiti cha enzi mbele za Mungu milele; amuru upendo wako na uaminifu wako vimlinde.
Agnanayonto nga agtalinaed isuna iti sangoanan ti Dios.
8 Ndipo daima nitaliimbia sifa jina lako na kuzitimiza nadhiri zangu siku baada ya siku.
Agnanayonto nga agkantaak iti pagdayaw iti naganmo tapno inaldaw a maaramidko dagiti sapatak.

< Zaburi 61 >