< Zaburi 61 >

1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za uimbaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, sikia kilio changu, usikilize maombi yangu.
למנצח על נגינת לדוד שמעה אלהים רנתי הקשיבה תפלתי׃
2 Kutoka miisho ya dunia ninakuita, ninaita huku moyo wangu unadhoofika; uniongoze kwenye mwamba ule ulio juu kuliko mimi.
מקצה הארץ אליך אקרא בעטף לבי בצור ירום ממני תנחני׃
3 Kwa kuwa umekuwa kimbilio langu, ngome imara dhidi ya adui.
כי היית מחסה לי מגדל עז מפני אויב׃
4 Natamani kukaa hemani mwako milele, na kukimbilia chini ya uvuli wa mbawa zako.
אגורה באהלך עולמים אחסה בסתר כנפיך סלה׃
5 Ee Mungu, kwa kuwa umesikia nadhiri zangu, umenipa urithi wa wale wanaoliogopa jina lako.
כי אתה אלהים שמעת לנדרי נתת ירשת יראי שמך׃
6 Mwongezee mfalme siku za maisha yake, miaka yake kwa vizazi vingi.
ימים על ימי מלך תוסיף שנותיו כמו דר ודר׃
7 Yeye na atawazwe kwenye kiti cha enzi mbele za Mungu milele; amuru upendo wako na uaminifu wako vimlinde.
ישב עולם לפני אלהים חסד ואמת מן ינצרהו׃
8 Ndipo daima nitaliimbia sifa jina lako na kuzitimiza nadhiri zangu siku baada ya siku.
כן אזמרה שמך לעד לשלמי נדרי יום יום׃

< Zaburi 61 >