< Zaburi 61 >

1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za uimbaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, sikia kilio changu, usikilize maombi yangu.
למנצח על-נגינת לדוד ב שמעה אלהים רנתי הקשיבה תפלתי
2 Kutoka miisho ya dunia ninakuita, ninaita huku moyo wangu unadhoofika; uniongoze kwenye mwamba ule ulio juu kuliko mimi.
מקצה הארץ אליך אקרא-- בעטף לבי בצור-ירום ממני תנחני
3 Kwa kuwa umekuwa kimbilio langu, ngome imara dhidi ya adui.
כי-היית מחסה לי מגדל-עז מפני אויב
4 Natamani kukaa hemani mwako milele, na kukimbilia chini ya uvuli wa mbawa zako.
אגורה באהלך עולמים אחסה בסתר כנפיך סלה
5 Ee Mungu, kwa kuwa umesikia nadhiri zangu, umenipa urithi wa wale wanaoliogopa jina lako.
כי-אתה אלהים שמעת לנדרי נתת ירשת יראי שמך
6 Mwongezee mfalme siku za maisha yake, miaka yake kwa vizazi vingi.
ימים על-ימי-מלך תוסיף שנותיו כמו-דר ודר
7 Yeye na atawazwe kwenye kiti cha enzi mbele za Mungu milele; amuru upendo wako na uaminifu wako vimlinde.
ישב עולם לפני אלהים חסד ואמת מן ינצרהו
8 Ndipo daima nitaliimbia sifa jina lako na kuzitimiza nadhiri zangu siku baada ya siku.
כן אזמרה שמך לעד-- לשלמי נדרי יום יום

< Zaburi 61 >