< Zaburi 61 >
1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za uimbaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, sikia kilio changu, usikilize maombi yangu.
“To the chief musician upon Neginah, by David.” Hear, O God, my entreaty; listen to my prayer.
2 Kutoka miisho ya dunia ninakuita, ninaita huku moyo wangu unadhoofika; uniongoze kwenye mwamba ule ulio juu kuliko mimi.
From the end of the earth will I call unto thee, when my heart is overwhelmed: lead me to the rock that is too high for me.
3 Kwa kuwa umekuwa kimbilio langu, ngome imara dhidi ya adui.
For thou hast been a shelter unto me, a strong tower against the enemy.
4 Natamani kukaa hemani mwako milele, na kukimbilia chini ya uvuli wa mbawa zako.
Let me sojourn in thy tent to all eternity; let me be sheltered under the covert of thy wings. (Selah)
5 Ee Mungu, kwa kuwa umesikia nadhiri zangu, umenipa urithi wa wale wanaoliogopa jina lako.
For thou, O God, hast truly listened to my vows: thou hast given back the heritage of those that fear thy name.
6 Mwongezee mfalme siku za maisha yake, miaka yake kwa vizazi vingi.
Oh, add days unto the king's days: may his years be as of many generations.
7 Yeye na atawazwe kwenye kiti cha enzi mbele za Mungu milele; amuru upendo wako na uaminifu wako vimlinde.
May he abide for ever before God: ordain that kindness and truth may guard him.
8 Ndipo daima nitaliimbia sifa jina lako na kuzitimiza nadhiri zangu siku baada ya siku.
So will I sing praise unto thy name for ever, that I may pay my vows day by day.