< Zaburi 61 >
1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za uimbaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, sikia kilio changu, usikilize maombi yangu.
Rhotoeng neh aka mawt ham David kah Pathen aw ka tamlung he ya lamtah ka thangthuinah he hnatung lah.
2 Kutoka miisho ya dunia ninakuita, ninaita huku moyo wangu unadhoofika; uniongoze kwenye mwamba ule ulio juu kuliko mimi.
Nang te Diklai a bawt lamkah kan khue. Ka lungbuei a rhae vaengah kamah lakah aka sang lungpang taengla kai nan mawt.
3 Kwa kuwa umekuwa kimbilio langu, ngome imara dhidi ya adui.
Kai ham tah hlipyingnah neh thunkha hmai ah sarhi rhaltoengim la na om.
4 Natamani kukaa hemani mwako milele, na kukimbilia chini ya uvuli wa mbawa zako.
Na dap khuiah kumhal ka bakuep vetih na phae hlip ah ka ying ni. (Selah)
5 Ee Mungu, kwa kuwa umesikia nadhiri zangu, umenipa urithi wa wale wanaoliogopa jina lako.
Pathen namah loh ka olcaeng te na yaak dongah na ming aka rhih tah rho na paek.
6 Mwongezee mfalme siku za maisha yake, miaka yake kwa vizazi vingi.
Manghai kah a tue khohnin te puh sak lamtah a kum khaw cadilcahma duela nguel sak.
7 Yeye na atawazwe kwenye kiti cha enzi mbele za Mungu milele; amuru upendo wako na uaminifu wako vimlinde.
Sitlohnah Pathen hmai ah kumhal khosa saeh lamtah a khueh oltak loh anih te kueinah saeh.
8 Ndipo daima nitaliimbia sifa jina lako na kuzitimiza nadhiri zangu siku baada ya siku.
Khohnin, khohnin ah ka olcaeng te thuung ham na ming ka tingtoeng yoeyah.