< Zaburi 60 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Shushani Eduthi.” Utenzi wa Daudi wa kufundisha. Wakati alipopigana na Waaramu kutoka Aramu-Naharaimu na Aramu-Soba, naye Yoabu akarudi nyuma na kuwaua Waedomu 12,000 katika Bonde la Chumvi. Ee Mungu, umetukataa na kutokea ghafula juu yetu, umekasirika: sasa turejeshe upya!
Para el músico principal. Con la melodía de “El Lirio de la Alianza”. Un poema didáctico de David, cuando luchó con Aram Naharaim y con Aram Zobah, y Joab volvió, y mató a doce mil de Edom en el Valle de la Sal. Dios, nos has rechazado. Nos has destrozado. Te has enfadado. Restablézcanos, de nuevo.
2 Umetetemesha nchi na kuipasua; uiponye mavunjiko yake, kwa maana inatetemeka.
Has hecho temblar la tierra. Lo has roto. Arreglar sus fracturas, porque tiembla.
3 Umewaonyesha watu wako nyakati za kukata tamaa; umetunywesha mvinyo unaotuyumbisha.
Has mostrado a tu pueblo cosas difíciles. Nos has hecho beber el vino que nos hace tambalear.
4 Kwa wale wanaokucha wewe, umewainulia bendera, ili iweze kutwekwa dhidi ya upinde.
Has dado un estandarte a los que te temen, para que se muestre por la verdad. (Selah)
5 Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
Para que tu amado sea liberado, salva con tu mano derecha, y respóndenos.
6 Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
Dios ha hablado desde su santuario: “Voy a triunfar. Dividiré Siquem, y medir el valle de Succoth.
7 Gileadi ni yangu na Manase ni yangu; Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
Mío es Galaad y mío es Manasés. Efraín también es la defensa de mi cabeza. Judá es mi cetro.
8 Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
Moab es mi lavabo. Lanzaré mi sandalia sobre Edom. Grito de triunfo sobre Filistea”.
9 Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
¿Quién me llevará a la ciudad fuerte? ¿Quién me ha llevado a Edom?
10 Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
¿No nos has rechazado, Dios, a nosotros? No sales con nuestros ejércitos, Dios.
11 Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
Danos ayuda contra el adversario, porque la ayuda del hombre es vana.
12 Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.
Por medio de Dios lo haremos con valentía, ya que es él quien va a pisotear a nuestros adversarios.

< Zaburi 60 >