< Zaburi 60 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Shushani Eduthi.” Utenzi wa Daudi wa kufundisha. Wakati alipopigana na Waaramu kutoka Aramu-Naharaimu na Aramu-Soba, naye Yoabu akarudi nyuma na kuwaua Waedomu 12,000 katika Bonde la Chumvi. Ee Mungu, umetukataa na kutokea ghafula juu yetu, umekasirika: sasa turejeshe upya!
ダビデ、ナハライムのアラムおよびゾバのアラムとたたかひをりしがヨアブかへりゆき塩谷にてエドム人一萬二千をころししとき教訓をなさんとてダビデがよみて「證詞の百合花」といふ調にあはせて伶長にうたはしめたるミクタムの歌 神よなんぢわれらを棄われらをちらし給へり なんぢは憤ほりたまへり ねがはくは再びわれらを歸したまへ
2 Umetetemesha nchi na kuipasua; uiponye mavunjiko yake, kwa maana inatetemeka.
なんぢ國をふるはせてこれを裂たまへり ねがはくはその多くの隙をおぎなひたまへ そは國ゆりうごくなり
3 Umewaonyesha watu wako nyakati za kukata tamaa; umetunywesha mvinyo unaotuyumbisha.
なんぢはその民にたへがたきことをしめし 人をよろめかする酒をわれらに飮しめ給へり
4 Kwa wale wanaokucha wewe, umewainulia bendera, ili iweze kutwekwa dhidi ya upinde.
なんぢ眞理のために挙しめんとて汝をおそるるものに一つの旗をあたへたまへり (セラ)
5 Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
ねがはくは右の手をもて救をほどこし われらに答をなして愛しみたまふものに助をえしめたまへ
6 Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
神はその聖をもていひたまへり われ甚くよろこばん われシケムをわかちスコテの谷をはからん
7 Gileadi ni yangu na Manase ni yangu; Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
ギレアデはわがもの マナセはわが有なり エフライムも亦わが首のまもりなり ユダはわが杖
8 Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
モアブはわが足盥なり エドムにはわが履をなげん ベリシテよわが故によりて聲をあげよと
9 Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
たれかわれを堅固なる邑にすすましめんや 誰かわれをみちびきてエドムにゆきたるか
10 Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
神よなんぢはわれらを棄たまひしにあらずや 神よなんぢはわれらの軍とともにいでゆきたまはず
11 Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
ねがはくは助をわれにあたへて敵にむかはしめたまへ 人のたすけは空しければなり
12 Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.
われらは神によりて勇しくはたらかん われらの敵をみたまふものは神なればなり

< Zaburi 60 >