< Zaburi 60 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Shushani Eduthi.” Utenzi wa Daudi wa kufundisha. Wakati alipopigana na Waaramu kutoka Aramu-Naharaimu na Aramu-Soba, naye Yoabu akarudi nyuma na kuwaua Waedomu 12,000 katika Bonde la Chumvi. Ee Mungu, umetukataa na kutokea ghafula juu yetu, umekasirika: sasa turejeshe upya!
“For the leader of the music; upon the Shushan-Eduth; a psalm of David for instruction; when he was at strife with the Syrians of Mesopotamia, and the Syrians of Zoba; when Joab returned, and smote twelve thousand Edomites in the valley of Salt.” O God! thou hast forsaken us; thou hast broken us in pieces; Thou hast been angry! O revive us again!
2 Umetetemesha nchi na kuipasua; uiponye mavunjiko yake, kwa maana inatetemeka.
Thou hast made the land tremble; thou hast rent it; O heal its breaches, for it tottereth!
3 Umewaonyesha watu wako nyakati za kukata tamaa; umetunywesha mvinyo unaotuyumbisha.
Thou hast caused thy people to see hard things; Thou hast made us drink the wine of reeling.
4 Kwa wale wanaokucha wewe, umewainulia bendera, ili iweze kutwekwa dhidi ya upinde.
Lift up a banner for them that fear thee, For the sake of thy faithfulness, that they may escape!
5 Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
That thy beloved may be delivered, Save with thy right hand, and answer me!
6 Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
God promiseth in his holiness; I will rejoice; I shall yet divide Shechem, And measure out the valley of Succoth.
7 Gileadi ni yangu na Manase ni yangu; Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
Gilead shall be mine, and mine Manasseh; Ephraim shall be my helmet, And Judah my sceptre;
8 Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
Moab shall be my wash-bowl; Upon Edom shall I cast my shoe; I shall triumph over Philistia!
9 Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
Who will bring me to the strong city? Who will lead me into Edom?
10 Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
Wilt not thou, O God! who didst forsake us, And didst not go forth with our armies?
11 Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
Give us thine aid in our distress, For vain is the help of man!
12 Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.
Through God we shall do valiantly; For he will tread down our enemies.

< Zaburi 60 >