< Zaburi 6 >
1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Mtindo wa sheminithi. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, usinikemee katika hasira yako, wala usiniadhibu katika ghadhabu yako.
Al Músico principal: en Neginoth sobre Seminith: Salmo de David. JEHOVÁ, no me reprendas en tu furor, ni me castigues con tu ira.
2 Unirehemu Bwana, kwa maana nimedhoofika; Ee Bwana, uniponye, kwa maana mifupa yangu ina maumivu makali.
Ten misericordia de mí, oh Jehová, porque yo estoy debilitado: sáname, oh Jehová, porque mis huesos están conmovidos.
3 Nafsi yangu ina uchungu mwingi. Mpaka lini, Ee Bwana, mpaka lini?
Mi alma asimismo está muy conturbada: y tú, Jehová, ¿hasta cuándo?
4 Geuka Ee Bwana, unikomboe, uniokoe kwa sababu ya fadhili zako.
Vuelve, oh Jehová, libra mi alma; sálvame por tu misericordia.
5 Hakuna mtu anayekukumbuka akiwa amekufa. Ni nani awezaye kukusifu akiwa kuzimu? (Sheol )
Porque en la muerte no hay memoria de ti: ¿quién te loará en el sepulcro? (Sheol )
6 Nimechakaa kwa kulia kwa huzuni; usiku kucha nafurikisha kitanda changu kwa machozi; nimelowesha viti vyangu vya fahari kwa machozi.
Heme consumido á fuerza de gemir: todas las noches inundo mi lecho, riego mi estrado con mis lágrimas.
7 Macho yangu yamedhoofika kwa kuhuzunika, yamedhoofika kwa sababu ya adui zangu wote.
Mis ojos están carcomidos de descontento; hanse envejecido á causa de todos mis angustiadores.
8 Kaeni mbali nami, ninyi nyote mtendao mabaya, kwa maana Bwana amesikia kulia kwangu.
Apartaos de mí, todos los obradores de iniquidad; porque Jehová ha oído la voz de mi lloro.
9 Bwana amesikia kilio changu kwa huruma, Bwana amekubali sala yangu.
Jehová ha oído mi ruego; ha recibido Jehová mi oración.
10 Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika, watarudi nyuma kwa aibu ya ghafula.
Se avergonzarán, y turbaránse mucho todos mis enemigos; volveránse y serán avergonzados subitáneamente.