< Zaburi 6 >

1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Mtindo wa sheminithi. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, usinikemee katika hasira yako, wala usiniadhibu katika ghadhabu yako.
Jehová, no me reprendas con tu furor: ni me castigues con tu ira.
2 Unirehemu Bwana, kwa maana nimedhoofika; Ee Bwana, uniponye, kwa maana mifupa yangu ina maumivu makali.
Ten misericordia de mí, o! Jehová, porque yo estoy debilitado: sáname, o! Jehová, porque mis huesos están conturbados.
3 Nafsi yangu ina uchungu mwingi. Mpaka lini, Ee Bwana, mpaka lini?
Y mi alma está muy conturbada: y tú, Jehová, ¿hasta cuándo?
4 Geuka Ee Bwana, unikomboe, uniokoe kwa sababu ya fadhili zako.
Vuelve, o! Jehová, escapa mi alma, sálvame por tu misericordia:
5 Hakuna mtu anayekukumbuka akiwa amekufa. Ni nani awezaye kukusifu akiwa kuzimu? (Sheol h7585)
Porque en la muerte no hay memoria de ti: en el sepulcro ¿quién te loará? (Sheol h7585)
6 Nimechakaa kwa kulia kwa huzuni; usiku kucha nafurikisha kitanda changu kwa machozi; nimelowesha viti vyangu vya fahari kwa machozi.
Trabajado he con mi gemido: toda la noche hago nadar mi cama en mis lágrimas: deslío mi estrado.
7 Macho yangu yamedhoofika kwa kuhuzunika, yamedhoofika kwa sababu ya adui zangu wote.
Mis ojos están carcomidos de descontento: hánse envejecido a causa de todos mis angustiadores.
8 Kaeni mbali nami, ninyi nyote mtendao mabaya, kwa maana Bwana amesikia kulia kwangu.
Apartáos de mí todos los obradores de iniquidad: porque Jehová ha oído la voz de mi lloro.
9 Bwana amesikia kilio changu kwa huruma, Bwana amekubali sala yangu.
Jehová ha oído mi ruego: Jehová ha recibido mi oración.
10 Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika, watarudi nyuma kwa aibu ya ghafula.
Avergonzarse han, y turbarse han mucho todos mis enemigos: volverán, y avergonzarse han súbitamente.

< Zaburi 6 >