< Zaburi 6 >

1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Mtindo wa sheminithi. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, usinikemee katika hasira yako, wala usiniadhibu katika ghadhabu yako.
For the Leader; with string-music; on the Sheminith. A Psalm of David. O LORD, rebuke me not in Thine anger, neither chasten me in Thy wrath.
2 Unirehemu Bwana, kwa maana nimedhoofika; Ee Bwana, uniponye, kwa maana mifupa yangu ina maumivu makali.
Be gracious unto me, O LORD, for I languish away; heal me, O LORD, for my bones are affrighted.
3 Nafsi yangu ina uchungu mwingi. Mpaka lini, Ee Bwana, mpaka lini?
My soul also is sore affrighted; and Thou, O LORD, how long?
4 Geuka Ee Bwana, unikomboe, uniokoe kwa sababu ya fadhili zako.
Return, O LORD, deliver my soul; save me for Thy mercy's sake.
5 Hakuna mtu anayekukumbuka akiwa amekufa. Ni nani awezaye kukusifu akiwa kuzimu? (Sheol h7585)
For in death there is no remembrance of Thee; in the nether-world who will give Thee thanks? (Sheol h7585)
6 Nimechakaa kwa kulia kwa huzuni; usiku kucha nafurikisha kitanda changu kwa machozi; nimelowesha viti vyangu vya fahari kwa machozi.
I am weary with my groaning; every night make I my bed to swim; I melt away my couch with my tears.
7 Macho yangu yamedhoofika kwa kuhuzunika, yamedhoofika kwa sababu ya adui zangu wote.
Mine eye is dimmed because of vexation; it waxeth old because of all mine adversaries.
8 Kaeni mbali nami, ninyi nyote mtendao mabaya, kwa maana Bwana amesikia kulia kwangu.
Depart from me, all ye workers of iniquity; for the LORD hath heard the voice of my weeping.
9 Bwana amesikia kilio changu kwa huruma, Bwana amekubali sala yangu.
The LORD hath heard my supplication; the LORD receiveth my prayer.
10 Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika, watarudi nyuma kwa aibu ya ghafula.
All mine enemies shall be ashamed and sore affrighted; they shall turn back, they shall be ashamed suddenly.

< Zaburi 6 >