< Zaburi 6 >

1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Mtindo wa sheminithi. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, usinikemee katika hasira yako, wala usiniadhibu katika ghadhabu yako.
For the choirmaster. With stringed instruments, according to Sheminith. A Psalm of David. O LORD, do not rebuke me in Your anger or discipline me in Your wrath.
2 Unirehemu Bwana, kwa maana nimedhoofika; Ee Bwana, uniponye, kwa maana mifupa yangu ina maumivu makali.
Be merciful to me, O LORD, for I am frail; heal me, O LORD, for my bones are in agony.
3 Nafsi yangu ina uchungu mwingi. Mpaka lini, Ee Bwana, mpaka lini?
My soul is deeply distressed. How long, O LORD, how long?
4 Geuka Ee Bwana, unikomboe, uniokoe kwa sababu ya fadhili zako.
Turn, O LORD, and deliver my soul; save me because of Your loving devotion.
5 Hakuna mtu anayekukumbuka akiwa amekufa. Ni nani awezaye kukusifu akiwa kuzimu? (Sheol h7585)
For there is no mention of You in death; who can praise You from Sheol? (Sheol h7585)
6 Nimechakaa kwa kulia kwa huzuni; usiku kucha nafurikisha kitanda changu kwa machozi; nimelowesha viti vyangu vya fahari kwa machozi.
I am weary from groaning; all night I flood my bed with weeping and drench my couch with tears.
7 Macho yangu yamedhoofika kwa kuhuzunika, yamedhoofika kwa sababu ya adui zangu wote.
My eyes fail from grief; they grow dim because of all my foes.
8 Kaeni mbali nami, ninyi nyote mtendao mabaya, kwa maana Bwana amesikia kulia kwangu.
Depart from me, all you workers of iniquity, for the LORD has heard my weeping.
9 Bwana amesikia kilio changu kwa huruma, Bwana amekubali sala yangu.
The LORD has heard my cry for mercy; the LORD accepts my prayer.
10 Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika, watarudi nyuma kwa aibu ya ghafula.
All my enemies will be ashamed and dismayed; they will turn back in sudden disgrace.

< Zaburi 6 >