< Zaburi 59 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Wakati Sauli alipotuma wapelelezi nyumbani mwa Daudi ili wamuue. Ee Mungu, uniokoe na adui zangu, unilinde kutokana na hao wanaoinuka dhidi yangu.
Escápame de mis enemigos, o! Dios mío: líbrame de los que se levantan contra mí.
2 Uniponye na watu watendao mabaya, uniokoe kutokana na wamwagao damu.
Escápame de los que obran iniquidad, y sálvame de los varones de sangres:
3 Tazama wanavyonivizia! Watu wakali wananifanyia hila, ingawa Ee Bwana, mimi sijakosea wala kutenda dhambi.
Porque, he aquí, han asechado a mi vida: hánse juntado contra mí fuertes sin rebelión mía, y sin pecado mío, o! Jehová.
4 Sijatenda kosa; hata hivyo wako tayari kunishambulia. Inuka unisaidie, uone hali yangu mbaya!
Sin mi delito corren, y se aperciben: despierta para encontrarme, y mira.
5 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli! Zinduka uyaadhibu mataifa yote, usionyeshe huruma kwa wasaliti.
Y tú, Jehová Dios de los ejércitos, Dios de Israel, despierta a visitar todas las naciones: no hayas misericordia de todos los que se rebelan con iniquidad. (Selah)
6 Hurudi wakati wa jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
Volverse han a la tarde, ladrarán como perros, y rodearán la ciudad.
7 Tazama yale wanayotema kutoka vinywa vyao, hutema upanga kutoka midomo yao, nao husema, “Ni nani atakayetusikia?”
He aquí, hablarán con su boca: espadas están en sus labios, porque, ¿Quién lo oye?
8 Lakini wewe, Bwana, uwacheke; unayadharau mataifa hayo yote.
Mas tú, Jehová, te reirás de ellos: harás burla de todas las gentes.
9 Ee nguvu yangu, ninakutazama wewe, wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,
Para ti reservaré su fortaleza: porque Dios es mi defensa.
10 Mungu wangu unipendaye. Mungu atanitangulia, naye atanifanya niwachekelee wale wanaonisingizia.
El Dios de mi misericordia me prevendrá: Dios me hará ver en mis enemigos venganza.
11 Lakini usiwaue, Ee Bwana, ngao yetu, au sivyo watu wangu watasahau. Katika uwezo wako wafanye watangetange na uwashushe chini.
No los matarás, porque mi pueblo no se olvide; házlos vagabundos con tu fortaleza, y abatelos, o! Jehová, escudo nuestro.
12 Kwa ajili ya dhambi za vinywa vyao, kwa ajili ya maneno ya midomo yao, waache wanaswe katika kiburi chao. Kwa ajili ya laana na uongo wanaotamka,
Por el pecado de su boca, por la palabra de sus labios, y sean presos por su soberbia: y cuenten de maldición y de enflaquecimiento,
13 wateketeze katika ghadhabu, wateketeze hadi wasiwepo tena. Ndipo itakapofahamika katika miisho ya dunia kwamba Mungu anatawala juu ya Yakobo.
Acába los con furor, acába los y no sean: y sepan que Dios domina en Jacob hasta los fines de la tierra. (Selah)
14 Hurudi jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
Y vuelvan a la tarde, y ladren como perros: y rodeen la ciudad.
15 Wanatangatanga wakitafuta chakula, wasipotosheka hubweka kama mbwa.
Anden ellos vagabundos para hallar que comer: y si no se hartaren, murmuren.
16 Lakini mimi nitaziimba nguvu zako, asubuhi nitaimba juu ya upendo wako; kwa maana wewe ndiwe ngome yangu na kimbilio langu wakati wa shida.
Y yo cantaré tu fortaleza y loaré de mañana tu misericordia: porque has sido mi amparo, y refugio en el día de mi angustia.
17 Ee uliye Nguvu zangu, ninakuimbia sifa. Wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu, Mungu unipendaye.
Fortaleza mía, a ti cantaré: porque eres Dios de mi amparo, Dios de mi misericordia.

< Zaburi 59 >