< Zaburi 59 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Wakati Sauli alipotuma wapelelezi nyumbani mwa Daudi ili wamuue. Ee Mungu, uniokoe na adui zangu, unilinde kutokana na hao wanaoinuka dhidi yangu.
Psalmus, in finem, ne corrumpas, David in tituli inscriptionem, quando misit Saul, et custodivit domum eius, ut eum interficeret. Eripe me de inimicis meis Deus meus: et ab insurgentibus in me libera me.
2 Uniponye na watu watendao mabaya, uniokoe kutokana na wamwagao damu.
Eripe me de operantibus iniquitatem: et de viris sanguinum salva me.
3 Tazama wanavyonivizia! Watu wakali wananifanyia hila, ingawa Ee Bwana, mimi sijakosea wala kutenda dhambi.
Quia ecce ceperunt animam meam: irruerunt in me fortes.
4 Sijatenda kosa; hata hivyo wako tayari kunishambulia. Inuka unisaidie, uone hali yangu mbaya!
Neque iniquitas mea, neque peccatum meum Domine: sine iniquitate cucurri, et direxi.
5 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli! Zinduka uyaadhibu mataifa yote, usionyeshe huruma kwa wasaliti.
Exurge in occursum meum, et vide: et tu Domine Deus virtutum, Deus Israel, Intende ad visitandas omnes gentes: non miserearis omnibus, qui operantur iniquitatem.
6 Hurudi wakati wa jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
Convertentur ad vesperam: et famem patientur ut canes, et circuibunt civitatem.
7 Tazama yale wanayotema kutoka vinywa vyao, hutema upanga kutoka midomo yao, nao husema, “Ni nani atakayetusikia?”
Ecce loquentur in ore suo, et gladius in labiis eorum: quoniam quis audivit?
8 Lakini wewe, Bwana, uwacheke; unayadharau mataifa hayo yote.
Et tu Domine deridebis eos: ad nihilum deduces omnes gentes.
9 Ee nguvu yangu, ninakutazama wewe, wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,
Fortitudinem meam ad te custodiam, quia Deus susceptor meus es:
10 Mungu wangu unipendaye. Mungu atanitangulia, naye atanifanya niwachekelee wale wanaonisingizia.
Deus meus misericordia eius praeveniet me.
11 Lakini usiwaue, Ee Bwana, ngao yetu, au sivyo watu wangu watasahau. Katika uwezo wako wafanye watangetange na uwashushe chini.
Deus ostendit mihi super inimicos meos, ne occidas eos: nequando obliviscantur populi mei. Disperge illos in virtute tua: et depone eos protector meus Domine:
12 Kwa ajili ya dhambi za vinywa vyao, kwa ajili ya maneno ya midomo yao, waache wanaswe katika kiburi chao. Kwa ajili ya laana na uongo wanaotamka,
Delictum oris eorum, sermonem labiorum ipsorum: et comprehendantur in superbia sua. Et de execratione et mendacio annunciabuntur
13 wateketeze katika ghadhabu, wateketeze hadi wasiwepo tena. Ndipo itakapofahamika katika miisho ya dunia kwamba Mungu anatawala juu ya Yakobo.
in consummatione: in ira consummationis, et non erunt. Et scient quia Deus dominabitur Iacob: et finium terrae.
14 Hurudi jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
Convertentur ad vesperam, et famem patientur ut canes: et circuibunt civitatem.
15 Wanatangatanga wakitafuta chakula, wasipotosheka hubweka kama mbwa.
Ipsi dispergentur ad manducandum: si vero non fuerint saturati, et murmurabunt.
16 Lakini mimi nitaziimba nguvu zako, asubuhi nitaimba juu ya upendo wako; kwa maana wewe ndiwe ngome yangu na kimbilio langu wakati wa shida.
Ego autem cantabo fortitudinem tuam: et exaltabo mane misericordiam tuam. Quia factus es susceptor meus, et refugium meum, in die tribulationis meae.
17 Ee uliye Nguvu zangu, ninakuimbia sifa. Wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu, Mungu unipendaye.
Adiutor meus tibi psallam, quia Deus susceptor meus es: Deus meus misericordia mea.

< Zaburi 59 >