< Zaburi 59 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Wakati Sauli alipotuma wapelelezi nyumbani mwa Daudi ili wamuue. Ee Mungu, uniokoe na adui zangu, unilinde kutokana na hao wanaoinuka dhidi yangu.
To the choirmaster al-tashcheth of David a miktam when sent Saul and people watched the house to kill him. Deliver me from enemies my - O God my from [those who] rise up against me may you set on high me.
2 Uniponye na watu watendao mabaya, uniokoe kutokana na wamwagao damu.
Deliver me from [those who] do wickedness and from men of blood save me.
3 Tazama wanavyonivizia! Watu wakali wananifanyia hila, ingawa Ee Bwana, mimi sijakosea wala kutenda dhambi.
For here! they lie in wait for life my they stir up trouble on me fierce [people] not transgression my and not sin my O Yahweh.
4 Sijatenda kosa; hata hivyo wako tayari kunishambulia. Inuka unisaidie, uone hali yangu mbaya!
Not iniquity they run! and they may be established awake! to meet me and see.
5 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli! Zinduka uyaadhibu mataifa yote, usionyeshe huruma kwa wasaliti.
And you O Yahweh God of - hosts [the] God of Israel awake! to punish all the nations may not you show favor to all [those who] act treacherously of wickedness (Selah)
6 Hurudi wakati wa jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
They return to evening they growl like dog so they may go around [the] city.
7 Tazama yale wanayotema kutoka vinywa vyao, hutema upanga kutoka midomo yao, nao husema, “Ni nani atakayetusikia?”
Here! - they pour forth! with mouth their swords [are] on lips their for who? [is] hearing.
8 Lakini wewe, Bwana, uwacheke; unayadharau mataifa hayo yote.
And you O Yahweh you laugh to them you mock all [the] nations.
9 Ee nguvu yangu, ninakutazama wewe, wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,
Strength his to you I will watch for God [is] refuge my.
10 Mungu wangu unipendaye. Mungu atanitangulia, naye atanifanya niwachekelee wale wanaonisingizia.
[the] God of (Covenant loyalty my *Q(K)*) he will meet me God he will let look me on enemies my.
11 Lakini usiwaue, Ee Bwana, ngao yetu, au sivyo watu wangu watasahau. Katika uwezo wako wafanye watangetange na uwashushe chini.
May not you kill them - lest they should forget people my make wander about them by strength your and bring down them O shield our O Lord.
12 Kwa ajili ya dhambi za vinywa vyao, kwa ajili ya maneno ya midomo yao, waache wanaswe katika kiburi chao. Kwa ajili ya laana na uongo wanaotamka,
[the] sin of Mouth their [the] word of lips their and let them be caught in pride their and from a curse and from lying [which] they speak.
13 wateketeze katika ghadhabu, wateketeze hadi wasiwepo tena. Ndipo itakapofahamika katika miisho ya dunia kwamba Mungu anatawala juu ya Yakobo.
Make an end in anger make an end and there not [will be] them so they may know that God [is] ruling over Jacob to [the] ends of the earth (Selah)
14 Hurudi jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
So they may return to evening they growl like dog so they may go around [the] city.
15 Wanatangatanga wakitafuta chakula, wasipotosheka hubweka kama mbwa.
They (they make wander about! *Q(K)*) to eat if not they are satisfied and they passed [the] night.
16 Lakini mimi nitaziimba nguvu zako, asubuhi nitaimba juu ya upendo wako; kwa maana wewe ndiwe ngome yangu na kimbilio langu wakati wa shida.
And I - I will sing strength your so I may sing for joy to the morning covenant loyalty your for you have been a refuge of me and a place of escape on [the] day [when] it is distress to me.
17 Ee uliye Nguvu zangu, ninakuimbia sifa. Wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu, Mungu unipendaye.
O strength my to you I will sing praises for God [is] refuge my [the] God of covenant loyalty my.

< Zaburi 59 >