< Zaburi 59 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Wakati Sauli alipotuma wapelelezi nyumbani mwa Daudi ili wamuue. Ee Mungu, uniokoe na adui zangu, unilinde kutokana na hao wanaoinuka dhidi yangu.
[For the Chief Musician. To the tune of "Do Not Destroy." A poem by David, when Saul sent, and they watched the house to kill him.] Deliver me from my enemies, my God. Set me on high from those who rise up against me.
2 Uniponye na watu watendao mabaya, uniokoe kutokana na wamwagao damu.
Deliver me from evildoers. Save me from the bloodthirsty men.
3 Tazama wanavyonivizia! Watu wakali wananifanyia hila, ingawa Ee Bwana, mimi sijakosea wala kutenda dhambi.
For, look, they lie in wait for my soul. The mighty gather themselves together against me, not for my disobedience, nor for my sin, LORD.
4 Sijatenda kosa; hata hivyo wako tayari kunishambulia. Inuka unisaidie, uone hali yangu mbaya!
I have done no wrong, yet they are ready to attack me. Rise up, look, and help me.
5 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli! Zinduka uyaadhibu mataifa yote, usionyeshe huruma kwa wasaliti.
You, LORD God of hosts, the God of Israel, rouse yourself to punish the nations. Show no mercy to the wicked traitors. (Selah)
6 Hurudi wakati wa jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
They return at evening, howling like dogs, and prowl around the city.
7 Tazama yale wanayotema kutoka vinywa vyao, hutema upanga kutoka midomo yao, nao husema, “Ni nani atakayetusikia?”
Look, they spew with their mouth. Swords are in their lips, "For," they say, "who hears us?"
8 Lakini wewe, Bwana, uwacheke; unayadharau mataifa hayo yote.
But you, LORD, laugh at them. You scoff at all the nations.
9 Ee nguvu yangu, ninakutazama wewe, wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,
Oh, my Strength, I watch for you, for God is my high tower.
10 Mungu wangu unipendaye. Mungu atanitangulia, naye atanifanya niwachekelee wale wanaonisingizia.
My God of mercy will come to meet me. God will let me look at my enemies in triumph.
11 Lakini usiwaue, Ee Bwana, ngao yetu, au sivyo watu wangu watasahau. Katika uwezo wako wafanye watangetange na uwashushe chini.
Do not kill them, or my people may forget. Scatter them by your power, and bring them down, LORD our shield.
12 Kwa ajili ya dhambi za vinywa vyao, kwa ajili ya maneno ya midomo yao, waache wanaswe katika kiburi chao. Kwa ajili ya laana na uongo wanaotamka,
For the sin of their mouth, and the words of their lips, let them be caught in their pride, for the curses and lies which they utter.
13 wateketeze katika ghadhabu, wateketeze hadi wasiwepo tena. Ndipo itakapofahamika katika miisho ya dunia kwamba Mungu anatawala juu ya Yakobo.
Consume them in wrath. Consume them, and they will be no more. Let them know that God rules in Jacob, to the farthest parts of the earth. (Selah)
14 Hurudi jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
At evening let them return. Let them howl like a dog, and go around the city.
15 Wanatangatanga wakitafuta chakula, wasipotosheka hubweka kama mbwa.
They shall wander up and down for food, and wait all night if they aren't satisfied.
16 Lakini mimi nitaziimba nguvu zako, asubuhi nitaimba juu ya upendo wako; kwa maana wewe ndiwe ngome yangu na kimbilio langu wakati wa shida.
But I will sing of your strength. Yes, I will sing aloud of your loving kindness in the morning. For you have been my high tower, a refuge in the day of my distress.
17 Ee uliye Nguvu zangu, ninakuimbia sifa. Wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu, Mungu unipendaye.
To you, my strength, I will sing praises. For God is my high tower, the God of my mercy.

< Zaburi 59 >