< Zaburi 59 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Wakati Sauli alipotuma wapelelezi nyumbani mwa Daudi ili wamuue. Ee Mungu, uniokoe na adui zangu, unilinde kutokana na hao wanaoinuka dhidi yangu.
“To the chief musician, Al-tashcheth, by David, a Michtham, when Saul sent, and they watched the house to put him to death.” Deliver me from my enemies, O my God: defend me from them that rise up against me.
2 Uniponye na watu watendao mabaya, uniokoe kutokana na wamwagao damu.
Deliver me from the workers of wickedness, and from men of blood do thou save me.
3 Tazama wanavyonivizia! Watu wakali wananifanyia hila, ingawa Ee Bwana, mimi sijakosea wala kutenda dhambi.
For, lo, they lie in wait for my soul, the mighty are gathered in troops against me: not for my transgression, nor for my sin, O Lord.
4 Sijatenda kosa; hata hivyo wako tayari kunishambulia. Inuka unisaidie, uone hali yangu mbaya!
Without guilt [in me] they run and make themselves ready: awake, [come] toward me, and behold.
5 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli! Zinduka uyaadhibu mataifa yote, usionyeshe huruma kwa wasaliti.
And thou, O Lord God of hosts, the God of Israel, awake to punish all the nations: be not gracious to any treacherous wicked one. (Selah)
6 Hurudi wakati wa jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
They will return at evening; they will howl like dogs, and go round about the city.
7 Tazama yale wanayotema kutoka vinywa vyao, hutema upanga kutoka midomo yao, nao husema, “Ni nani atakayetusikia?”
Behold, they sputter with their mouth: swords are in their lips; for who, [say they, ] doth hear?
8 Lakini wewe, Bwana, uwacheke; unayadharau mataifa hayo yote.
But thou, O Lord, wilt laugh at theme: thou wilt hold in derision all the nations.
9 Ee nguvu yangu, ninakutazama wewe, wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,
Because of [the enemy's] strength will I wait upon thee; for God is my defence.
10 Mungu wangu unipendaye. Mungu atanitangulia, naye atanifanya niwachekelee wale wanaonisingizia.
The God who showeth me kindness will go before me: God will let me see [my desire] upon those who regard me with envy.
11 Lakini usiwaue, Ee Bwana, ngao yetu, au sivyo watu wangu watasahau. Katika uwezo wako wafanye watangetange na uwashushe chini.
Slay them not, that my people may not forget: drive them about by thy power; and bring them down, thou our shield, O Lord.
12 Kwa ajili ya dhambi za vinywa vyao, kwa ajili ya maneno ya midomo yao, waache wanaswe katika kiburi chao. Kwa ajili ya laana na uongo wanaotamka,
The sin of their mouth is the word of their lips: let them be caught through their pride, because of the cursing and lying which they relate.
13 wateketeze katika ghadhabu, wateketeze hadi wasiwepo tena. Ndipo itakapofahamika katika miisho ya dunia kwamba Mungu anatawala juu ya Yakobo.
Make an end in fury, make an end [of them], that they my be no more, and let them know that God ruleth in Jacob, as far as the ends of the earth. (Selah)
14 Hurudi jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
And they will return in the evening; they will howl like dogs, and go round about the city.
15 Wanatangatanga wakitafuta chakula, wasipotosheka hubweka kama mbwa.
They will indeed roam about after something to eat, if they be not satisfied, so that they can be at rest.
16 Lakini mimi nitaziimba nguvu zako, asubuhi nitaimba juu ya upendo wako; kwa maana wewe ndiwe ngome yangu na kimbilio langu wakati wa shida.
But I will truly sing of thy strength; yea, I will sing joyfully in the morning of thy kindness; for thou hast been a defence unto me and a refuge on the day when I was distressed.
17 Ee uliye Nguvu zangu, ninakuimbia sifa. Wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu, Mungu unipendaye.
Unto thee, O my strength, will I sing; for God is my defence, the God of my kindness.

< Zaburi 59 >