< Zaburi 59 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Wakati Sauli alipotuma wapelelezi nyumbani mwa Daudi ili wamuue. Ee Mungu, uniokoe na adui zangu, unilinde kutokana na hao wanaoinuka dhidi yangu.
For the Leader; Al-tashheth. A Psalm of David; Michtam; when Saul sent, and they watched the house to kill him. Deliver me from mine enemies, O my God; set me on high from them that rise up against me.
2 Uniponye na watu watendao mabaya, uniokoe kutokana na wamwagao damu.
Deliver me from the workers of iniquity, and save me from the men of blood.
3 Tazama wanavyonivizia! Watu wakali wananifanyia hila, ingawa Ee Bwana, mimi sijakosea wala kutenda dhambi.
For, lo, they lie in wait for my soul; the impudent gather themselves together against me; not for my transgression, nor for my sin, O LORD.
4 Sijatenda kosa; hata hivyo wako tayari kunishambulia. Inuka unisaidie, uone hali yangu mbaya!
Without my fault, they run and prepare themselves; awake Thou to help me, and behold.
5 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli! Zinduka uyaadhibu mataifa yote, usionyeshe huruma kwa wasaliti.
Thou therefore, O LORD God of hosts, the God of Israel, arouse Thyself to punish all the nations; show no mercy to any iniquitous traitors. (Selah)
6 Hurudi wakati wa jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
They return at evening, they howl like a dog, and go round about the city.
7 Tazama yale wanayotema kutoka vinywa vyao, hutema upanga kutoka midomo yao, nao husema, “Ni nani atakayetusikia?”
Behold, they belch out with their mouth; swords are in their lips: 'For who doth hear?'
8 Lakini wewe, Bwana, uwacheke; unayadharau mataifa hayo yote.
But Thou, O LORD, shalt laugh at them; Thou shalt have all the nations in derision.
9 Ee nguvu yangu, ninakutazama wewe, wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,
Because of his strength, I will wait for Thee; for God is my high tower.
10 Mungu wangu unipendaye. Mungu atanitangulia, naye atanifanya niwachekelee wale wanaonisingizia.
The God of my mercy will come to meet me; God will let me gaze upon mine adversaries.
11 Lakini usiwaue, Ee Bwana, ngao yetu, au sivyo watu wangu watasahau. Katika uwezo wako wafanye watangetange na uwashushe chini.
Slay them not, lest my people forget, make them wander to and fro by Thy power, and bring them down, O Lord our shield.
12 Kwa ajili ya dhambi za vinywa vyao, kwa ajili ya maneno ya midomo yao, waache wanaswe katika kiburi chao. Kwa ajili ya laana na uongo wanaotamka,
For the sin of their mouth, and the words of their lips, let them even be taken in their pride, and for cursing and lying which they speak.
13 wateketeze katika ghadhabu, wateketeze hadi wasiwepo tena. Ndipo itakapofahamika katika miisho ya dunia kwamba Mungu anatawala juu ya Yakobo.
Consume them in wrath, consume them, that they be no more; and let them know that God ruleth in Jacob, unto the ends of the earth. (Selah)
14 Hurudi jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
And they return at evening, they howl like a dog, and go round about the city;
15 Wanatangatanga wakitafuta chakula, wasipotosheka hubweka kama mbwa.
They wander up and down to devour, and tarry all night if they have not their fill.
16 Lakini mimi nitaziimba nguvu zako, asubuhi nitaimba juu ya upendo wako; kwa maana wewe ndiwe ngome yangu na kimbilio langu wakati wa shida.
But as for me, I will sing of Thy strength; yea, I will sing aloud of Thy mercy in the morning; for Thou hast been my high tower, and a refuge in the day of my distress.
17 Ee uliye Nguvu zangu, ninakuimbia sifa. Wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu, Mungu unipendaye.
O my strength, unto Thee will I sing praises; for God is my high tower, the God of my mercy.

< Zaburi 59 >