< Zaburi 59 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Wakati Sauli alipotuma wapelelezi nyumbani mwa Daudi ili wamuue. Ee Mungu, uniokoe na adui zangu, unilinde kutokana na hao wanaoinuka dhidi yangu.
To him that excelleth. Destroy not. A Psalme of David on Michtam. When Saul sent and they did watch the house to kill him. O my God, deliuer mee from mine enemies: defend me from them that rise vp against me.
2 Uniponye na watu watendao mabaya, uniokoe kutokana na wamwagao damu.
Deliuer me from the wicked doers, and saue me from the bloody men.
3 Tazama wanavyonivizia! Watu wakali wananifanyia hila, ingawa Ee Bwana, mimi sijakosea wala kutenda dhambi.
For loe, they haue layd waite for my soule: the mightie men are gathered against me, not for mine offence, nor for my sinne, O Lord.
4 Sijatenda kosa; hata hivyo wako tayari kunishambulia. Inuka unisaidie, uone hali yangu mbaya!
They runne and prepare themselues without a fault on my part: arise therefore to assist me, and beholde.
5 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli! Zinduka uyaadhibu mataifa yote, usionyeshe huruma kwa wasaliti.
Euen thou, O Lord God of hostes, O God of Israel awake to visit all the heathen, and be not merciful vnto all that transgresse maliciously. (Selah)
6 Hurudi wakati wa jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
They goe to and from in the euening: they barke like dogs, and goe about the citie.
7 Tazama yale wanayotema kutoka vinywa vyao, hutema upanga kutoka midomo yao, nao husema, “Ni nani atakayetusikia?”
Behold, they brag in their talke, and swords are in their lips: for, Who, say they, doeth heare?
8 Lakini wewe, Bwana, uwacheke; unayadharau mataifa hayo yote.
But thou, O Lord, shalt haue them in derision, and thou shalt laugh at all the heathen.
9 Ee nguvu yangu, ninakutazama wewe, wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,
He is strong: but I will waite vpon thee: for God is my defence.
10 Mungu wangu unipendaye. Mungu atanitangulia, naye atanifanya niwachekelee wale wanaonisingizia.
My mercifull God will preuent me: God wil let me see my desire vpon mine enemies.
11 Lakini usiwaue, Ee Bwana, ngao yetu, au sivyo watu wangu watasahau. Katika uwezo wako wafanye watangetange na uwashushe chini.
Slay them not, least my people forget it: but scatter them abroad by thy power, and put them downe, O Lord our shield,
12 Kwa ajili ya dhambi za vinywa vyao, kwa ajili ya maneno ya midomo yao, waache wanaswe katika kiburi chao. Kwa ajili ya laana na uongo wanaotamka,
For the sinne of their mouth, and the words of their lips: and let them be taken in their pride, euen for their periurie and lies, that they speake.
13 wateketeze katika ghadhabu, wateketeze hadi wasiwepo tena. Ndipo itakapofahamika katika miisho ya dunia kwamba Mungu anatawala juu ya Yakobo.
Consume them in thy wrath: consume them that they be no more: and let them knowe that God ruleth in Iaakob, euen vnto the ends of the world. (Selah)
14 Hurudi jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
And in the euening they shall go to and from, and barke like dogs, and go about the citie.
15 Wanatangatanga wakitafuta chakula, wasipotosheka hubweka kama mbwa.
They shall runne here and there for meate: and surely they shall not be satisfied, though they tary all night.
16 Lakini mimi nitaziimba nguvu zako, asubuhi nitaimba juu ya upendo wako; kwa maana wewe ndiwe ngome yangu na kimbilio langu wakati wa shida.
But I wil sing of thy power, and will prayse thy mercy in the morning: for thou hast bene my defence and refuge in the day of my trouble.
17 Ee uliye Nguvu zangu, ninakuimbia sifa. Wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu, Mungu unipendaye.
Vnto thee, O my Strength, wil I sing: for God is my defence, and my mercifull God.

< Zaburi 59 >