< Zaburi 59 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Wakati Sauli alipotuma wapelelezi nyumbani mwa Daudi ili wamuue. Ee Mungu, uniokoe na adui zangu, unilinde kutokana na hao wanaoinuka dhidi yangu.
Unto the end, destroy not, for David for an inscription of It title, when Saul sent and watched his house to kill him. Deliver me from my enemies, O my God; and defend me from them that rise up against me.
2 Uniponye na watu watendao mabaya, uniokoe kutokana na wamwagao damu.
Deliver me from them that work iniquity, and save me from bloody men.
3 Tazama wanavyonivizia! Watu wakali wananifanyia hila, ingawa Ee Bwana, mimi sijakosea wala kutenda dhambi.
For behold they have caught my soul: the mighty have rushed in upon me:
4 Sijatenda kosa; hata hivyo wako tayari kunishambulia. Inuka unisaidie, uone hali yangu mbaya!
Neither is it my iniquity, nor my sin, O Lord: without iniquity have I run, and directed my steps.
5 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli! Zinduka uyaadhibu mataifa yote, usionyeshe huruma kwa wasaliti.
Rise up thou to meet me, and behold: even thou, O Lord, the God of hosts, the God of Israel. Attend to visit all the nations: have no mercy on all them that work iniquity.
6 Hurudi wakati wa jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
They shall return at evening, and shall suffer hunger like dogs: and shall go round about the city.
7 Tazama yale wanayotema kutoka vinywa vyao, hutema upanga kutoka midomo yao, nao husema, “Ni nani atakayetusikia?”
Behold they shall speak with their mouth, and a sword is in their lips: for who, say they, hath heard us?
8 Lakini wewe, Bwana, uwacheke; unayadharau mataifa hayo yote.
But thou, O Lord, shalt laugh at them: thou shalt bring all the nations to nothing.
9 Ee nguvu yangu, ninakutazama wewe, wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,
I will keep my strength to thee: for thou art my protector:
10 Mungu wangu unipendaye. Mungu atanitangulia, naye atanifanya niwachekelee wale wanaonisingizia.
My God, his mercy shall prevent me.
11 Lakini usiwaue, Ee Bwana, ngao yetu, au sivyo watu wangu watasahau. Katika uwezo wako wafanye watangetange na uwashushe chini.
God shall let me see over my enemies: slay them not, lest at any time my people forget. Scatter them by thy power; and bring them down, O Lord, my protector:
12 Kwa ajili ya dhambi za vinywa vyao, kwa ajili ya maneno ya midomo yao, waache wanaswe katika kiburi chao. Kwa ajili ya laana na uongo wanaotamka,
For the sin of their mouth, and the word of their lips: and let them be taken in their pride. And for their cursing and lying they shall be talked of,
13 wateketeze katika ghadhabu, wateketeze hadi wasiwepo tena. Ndipo itakapofahamika katika miisho ya dunia kwamba Mungu anatawala juu ya Yakobo.
When they are consumed: when they are consumed by thy wrath, and they shall be no more. And they shall know that God will rule Jacob, and all the ends of the earth.
14 Hurudi jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
They shall return at evening and shall suffer hunger like dogs: and shall go round about the city.
15 Wanatangatanga wakitafuta chakula, wasipotosheka hubweka kama mbwa.
They shall be scattered abroad to eat, and shall murmur if they be not filled.
16 Lakini mimi nitaziimba nguvu zako, asubuhi nitaimba juu ya upendo wako; kwa maana wewe ndiwe ngome yangu na kimbilio langu wakati wa shida.
But I will sing thy strength: and will extol thy mercy in the morning. For thou art become my support, and my refuge, in the day of my trouble.
17 Ee uliye Nguvu zangu, ninakuimbia sifa. Wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu, Mungu unipendaye.
Unto thee, O my helper, will I sing, for thou art God my defence: my God my mercy.

< Zaburi 59 >