< Zaburi 59 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Wakati Sauli alipotuma wapelelezi nyumbani mwa Daudi ili wamuue. Ee Mungu, uniokoe na adui zangu, unilinde kutokana na hao wanaoinuka dhidi yangu.
扫罗打发人窥探大卫的房屋,要杀他。那时,大卫作这金诗,交与伶长。调用休要毁坏。 我的 神啊,求你救我脱离仇敌, 把我安置在高处,得脱那些起来攻击我的人。
2 Uniponye na watu watendao mabaya, uniokoe kutokana na wamwagao damu.
求你救我脱离作孽的人 和喜爱流人血的人!
3 Tazama wanavyonivizia! Watu wakali wananifanyia hila, ingawa Ee Bwana, mimi sijakosea wala kutenda dhambi.
因为,他们埋伏要害我的命; 有能力的人聚集来攻击我。 耶和华啊,这不是为我的过犯, 也不是为我的罪愆。
4 Sijatenda kosa; hata hivyo wako tayari kunishambulia. Inuka unisaidie, uone hali yangu mbaya!
我虽然无过,他们预备整齐,跑来攻击我。 求你兴起鉴察,帮助我!
5 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli! Zinduka uyaadhibu mataifa yote, usionyeshe huruma kwa wasaliti.
万军之 神—耶和华以色列的 神啊! 求你兴起,惩治万邦! 不要怜悯行诡诈的恶人! (细拉)
6 Hurudi wakati wa jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
他们晚上转回, 叫号如狗,围城绕行。
7 Tazama yale wanayotema kutoka vinywa vyao, hutema upanga kutoka midomo yao, nao husema, “Ni nani atakayetusikia?”
他们口中喷吐恶言,嘴里有刀; 他们说:有谁听见?
8 Lakini wewe, Bwana, uwacheke; unayadharau mataifa hayo yote.
但你—耶和华必笑话他们; 你要嗤笑万邦。
9 Ee nguvu yangu, ninakutazama wewe, wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,
我的力量啊,我必仰望你, 因为 神是我的高台。
10 Mungu wangu unipendaye. Mungu atanitangulia, naye atanifanya niwachekelee wale wanaonisingizia.
我的 神要以慈爱迎接我; 神要叫我看见我仇敌遭报。
11 Lakini usiwaue, Ee Bwana, ngao yetu, au sivyo watu wangu watasahau. Katika uwezo wako wafanye watangetange na uwashushe chini.
不要杀他们,恐怕我的民忘记。 主啊,你是我们的盾牌; 求你用你的能力使他们四散, 且降为卑。
12 Kwa ajili ya dhambi za vinywa vyao, kwa ajili ya maneno ya midomo yao, waache wanaswe katika kiburi chao. Kwa ajili ya laana na uongo wanaotamka,
因他们口中的罪和嘴里的言语, 并咒骂虚谎的话, 愿他们在骄傲之中被缠住了。
13 wateketeze katika ghadhabu, wateketeze hadi wasiwepo tena. Ndipo itakapofahamika katika miisho ya dunia kwamba Mungu anatawala juu ya Yakobo.
求你发怒,使他们消灭, 以致归于无有, 叫他们知道 神在雅各中间掌权, 直到地极。 (细拉)
14 Hurudi jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
到了晚上,任凭他们转回; 任凭他们叫号如狗,围城绕行。
15 Wanatangatanga wakitafuta chakula, wasipotosheka hubweka kama mbwa.
他们必走来走去,寻找食物, 若不得饱就终夜在外。
16 Lakini mimi nitaziimba nguvu zako, asubuhi nitaimba juu ya upendo wako; kwa maana wewe ndiwe ngome yangu na kimbilio langu wakati wa shida.
但我要歌颂你的力量, 早晨要高唱你的慈爱; 因为你作过我的高台, 在我急难的日子作过我的避难所。
17 Ee uliye Nguvu zangu, ninakuimbia sifa. Wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu, Mungu unipendaye.
我的力量啊,我要歌颂你; 因为 神是我的高台, 是赐恩与我的 神。