< Zaburi 59 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Wakati Sauli alipotuma wapelelezi nyumbani mwa Daudi ili wamuue. Ee Mungu, uniokoe na adui zangu, unilinde kutokana na hao wanaoinuka dhidi yangu.
NALIBREYO gui enemigujo sija, O Yuusso; polo yo gui jilo guinin ayosija ni y mangajujulo contra guajo.
2 Uniponye na watu watendao mabaya, uniokoe kutokana na wamwagao damu.
Nalibreyo gui chumogüe y tinaelaye, ya satbayo gui manmejga na taotao sija.
3 Tazama wanavyonivizia! Watu wakali wananifanyia hila, ingawa Ee Bwana, mimi sijakosea wala kutenda dhambi.
Sa, estagüe, na mananangga y antijo: y manmetgot mandaña contra guajo; ti pot y tinaelayeco, ni ti pot y isaojo, O Jeova.
4 Sijatenda kosa; hata hivyo wako tayari kunishambulia. Inuka unisaidie, uone hali yangu mbaya!
Manmalago ya japrepara sija, sin y linachijo; fagmata, ya unayudayo, ya unlie.
5 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli! Zinduka uyaadhibu mataifa yote, usionyeshe huruma kwa wasaliti.
Jago Jeova, Yuus y inetnon sendalo, si Yuus Israel; fagmata ya unbisita todo y nasion sija; chamo gagaease ni y manaelaye. (Sila)
6 Hurudi wakati wa jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
Manalo guato yan pupuenge: ya manboruruca taegüije y galago, ya malilicucue y siuda.
7 Tazama yale wanayotema kutoka vinywa vyao, hutema upanga kutoka midomo yao, nao husema, “Ni nani atakayetusikia?”
Liija, sa mannutugap juyong guinin y pachotñija: espada sija guaja gui jalom labiosñija; jaye, ilegñiñija, cao jajungog?
8 Lakini wewe, Bwana, uwacheke; unayadharau mataifa hayo yote.
Lao jago, O Jeova, siempre unchatgue sija; siempre unmofea todo y nasion.
9 Ee nguvu yangu, ninakutazama wewe, wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,
O minetgotto, junanangga jao; sa si Yuus y guimajo lumijing.
10 Mungu wangu unipendaye. Mungu atanitangulia, naye atanifanya niwachekelee wale wanaonisingizia.
Si Yuusso nu y minaaseña, ugaegue gui menajo: si Yuus unaliiyo y minalagojo, gui jilo y enemigujo sija.
11 Lakini usiwaue, Ee Bwana, ngao yetu, au sivyo watu wangu watasahau. Katika uwezo wako wafanye watangetange na uwashushe chini.
Chamo pumupuno sija, sa trabia ti manmalelefa y taotaojo; chalapon sija pot y ninasiñamo; ya unchule sija papa, O Jeova, patangmame.
12 Kwa ajili ya dhambi za vinywa vyao, kwa ajili ya maneno ya midomo yao, waache wanaswe katika kiburi chao. Kwa ajili ya laana na uongo wanaotamka,
Pot y isao y pachotñija, yan pot y sinangan y labiosñija, polo ya ufanmacone, pot y sobetbioñija: yan pot y matdision, yan manmandadague ni y sinanganñija.
13 wateketeze katika ghadhabu, wateketeze hadi wasiwepo tena. Ndipo itakapofahamika katika miisho ya dunia kwamba Mungu anatawala juu ya Yakobo.
Lachae sija ni y binibumo, lachae sija, para sija ti ufangaegue talo: ya ujatungo na si Yuus mangobiebietna gui as Jacob, asta y uttimon y tano. (Sila)
14 Hurudi jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
Ya an pupuenge, polo ya ufanalo guato, ya unfanboruca taegüije y galago ya umalilicue y siuda.
15 Wanatangatanga wakitafuta chakula, wasipotosheka hubweka kama mbwa.
Nafanjajanao julo yan papa, ya ufanmanaliligao nañija; ya usaga todo puenge yanguin ti manjaspog.
16 Lakini mimi nitaziimba nguvu zako, asubuhi nitaimba juu ya upendo wako; kwa maana wewe ndiwe ngome yangu na kimbilio langu wakati wa shida.
Lao guajo, jucanta ni y ninasiñamo; magajet, na jucanta agang ni y minaasemo yan ogaan; sa guinin jago y guimajo lumijing, yan y guinegüeco gui jaanen chinatsagaco.
17 Ee uliye Nguvu zangu, ninakuimbia sifa. Wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu, Mungu unipendaye.
Jago, O minetgotjo, jucantaye y alabansa sija; sa si Yuus y guimajo lumijing, yan y Yuus y minaasejo.

< Zaburi 59 >