< Zaburi 57 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Baada ya kumponyoka Sauli pangoni. Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie, kwa maana nafsi yangu inakukimbilia. Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia mpaka maafa yapite.
למנצח אל-תשחת לדוד מכתם-- בברחו מפני-שאול במערה ב חנני אלהים חנני-- כי בך חסיה נפשי ובצל-כנפיך אחסה-- עד יעבר הוות
2 Namlilia Mungu Aliye Juu Sana, Mungu atimizaye makusudi yake kwangu.
אקרא לאלהים עליון לאל גמר עלי
3 Hutumana kutoka mbinguni na kuniokoa, akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali; Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.
ישלח משמים ויושיעני-- חרף שאפי סלה ישלח אלהים חסדו ואמתו
4 Niko katikati ya simba, nimelala katikati ya wanyama wenye njaa kuu: watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, ambao ndimi zao ni panga kali.
נפשי בתוך לבאם-- אשכבה להטים בני-אדם--שניהם חנית וחצים ולשונם חרב חדה
5 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
רומה על-השמים אלהים על כל-הארץ כבודך
6 Waliitegea miguu yangu nyavu, nikainamishwa chini na dhiki. Wamechimba shimo katika njia yangu, lakini wametumbukia humo wao wenyewe.
רשת הכינו לפעמי-- כפף נפשי כרו לפני שיחה נפלו בתוכה סלה
7 Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
נכון לבי אלהים נכון לבי אשירה ואזמרה
8 Amka, nafsi yangu! Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
עורה כבודי--עורה הנבל וכנור אעירה שחר
9 Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
אודך בעמים אדני אזמרך בלאמים
10 Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni, uaminifu wako unazifikia anga.
כי-גדל עד-שמים חסדך ועד-שחקים אמתך
11 Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni, utukufu wako na uwe duniani pote.
רומה על-שמים אלהים על כל-הארץ כבודך

< Zaburi 57 >