< Zaburi 57 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Baada ya kumponyoka Sauli pangoni. Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie, kwa maana nafsi yangu inakukimbilia. Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia mpaka maafa yapite.
Pour le chef musicien. Sur l'air de « Do Not Destroy ». Un poème de David, quand il fuyait Saül, dans la grotte. Soyez miséricordieux envers moi, Dieu, soyez miséricordieux envers moi, car mon âme se réfugie en toi. Oui, à l'ombre de tes ailes, je me réfugie, jusqu'à ce que le désastre soit passé.
2 Namlilia Mungu Aliye Juu Sana, Mungu atimizaye makusudi yake kwangu.
Je crie vers le Dieu Très Haut, à Dieu qui accomplit mes demandes pour moi.
3 Hutumana kutoka mbinguni na kuniokoa, akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali; Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.
Il enverra du ciel, et me sauvera, il réprimande celui qui me poursuit. (Selah) Dieu enverra sa bonté et sa vérité.
4 Niko katikati ya simba, nimelala katikati ya wanyama wenye njaa kuu: watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, ambao ndimi zao ni panga kali.
Mon âme est parmi les lions. Je me trouve parmi ceux qui sont incendiés, même les fils des hommes, dont les dents sont des lances et des flèches, et leur langue une épée tranchante.
5 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
Sois exalté, Dieu, au-dessus des cieux! Que ta gloire soit au-dessus de toute la terre!
6 Waliitegea miguu yangu nyavu, nikainamishwa chini na dhiki. Wamechimba shimo katika njia yangu, lakini wametumbukia humo wao wenyewe.
Ils ont préparé un filet pour mes pas. Mon âme s'est inclinée. Ils creusent une fosse devant moi. Ils tombent eux-mêmes au milieu de tout ça. (Selah)
7 Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
Mon cœur est inébranlable, Dieu. Mon cœur est inébranlable. Je vais chanter, oui, je vais chanter des louanges.
8 Amka, nafsi yangu! Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
Réveille-toi, ma gloire! Réveille-toi, luth et harpe! Je vais réveiller l'aube.
9 Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
Je te louerai, Seigneur, parmi les peuples. Je chanterai tes louanges parmi les nations.
10 Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni, uaminifu wako unazifikia anga.
Car ta grande bonté atteint les cieux, et votre vérité dans les cieux.
11 Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni, utukufu wako na uwe duniani pote.
Sois exalté, Dieu, au-dessus des cieux. Que ta gloire soit sur toute la terre.

< Zaburi 57 >